04/01/2021
IKO WAPI ZAMANI?
✏ Zamani nyumba zetu zilikuwa na vyumba vichache na sehemu ya kukaa tu, tunakutana ndugu, jamaa na majirani.
✏ Lakini leo nyumba zetu kubwa na zina vyumba vingi, isipokuwa hazina watu ila ardhi na kuta tu.
✏ Huyu kasafiri na yule kajilipuwa nchi nyingine, huyu kakasirika haongei na mtu na mwingine yupo hoi na Dunia.
✏ Zamani chakula chetu ni wali, mihogo, ndizi, magimbi, dagaa, au ugali kwa Mchicha.
✏ Tunatandika mkeka au jamvi chini na tunakula sahani moja sote, tunacheka kwa furaha mpaka jirani wanatusikia.
✏ Lakini leo hii sufuria au hotpot imejaa nyama, kuku na minofu ya samaki na kila mmoja na sahani yake ya aina tofauti .
✏ Basi mnakaa sehemu zipo tupu, unatamani ndugu au jirani wawepo, wazibe hilo pengo.
✏ Zamani tunakaa uwani na babu, anatuhadithia hadithi, tunakunywa chai kwa upendo na kucheka kwa pamoja kwa tabasamu mpaka meno yetu yanaonekana.
✏ Na leo kukaa kwetu ni kwenye simu za mkononi, internet na kuchat tu kwenye whatsApp,Imo, instagram, facebook na mitandao mingine ya kijamii, tumekuwa tupo kwingine kabisa.
✏ Zamani tunauliziana, kujuliana hali, kutembeleana, na tunakutana kwa furaha na kukumbatiana.
✏ Leo ni sikukuu mpaka sikukuu au harusi hadi harusi au mpaka kuwe na maziko ndiyo tunatembeleana au kuonana tena kwa kujilazimisha, hata salaam ya mungu hatusalimiani, na kukaa kwetu kwa mioyo ya moto.
✏ Zamani mtu akiumwa kati yetu, tunakusanyika ndugu na majirani.
✏ Leo ndugu hakujali, hana muda na wewe na anakuambia niwahi mimi taabani hoi.
✏ Zamani ilikua ndugu anamuenzi ndugu yake na dada yake, kwa kila alichonacho hata k**a kachoka au ana stress.
✏ Leo unamkuta mtu hapati kula na ndugu yake yupo kazama katika neema, anajifanya kakasirika kwa sababu za kijinga, na kukata mawasiliano kwa miaka.
✏ Leo pesa inabadili nafsi ya mtu, hajali ndugu wala jirani, utu unapotea anasahau k**a kuna kufa au Dunia ina mwisho .
✏ Mpo wapi watu wa zamani mje muone vipi mioyo ilivyo kati ya ndugu leo hii..!!
✏ Miaka na siku hazirudi nyuma, tenda wema uende zako usingoje shukrani.
✏ Unasaidia ndugu au mtu shukrani yake katika ulimi tu, lakini moyoni mwake kuna moto anasahau ihsani na kukusema kwa vibaya mno.
✏ Hamna tena undugu wa kuwakusanya pamoja k**a zamani, hamna mapenzi na upendo ndani ya mioyo, (hata heshima kwa mkubwa k**a zamani hamna).
✏ Iko wapi zamani? Mola awarehemu wa zamani waliotangulia.
Mola atujaaliye tuwe wenye kupendana na kushik**ana kwa kila hali k**a ilivyokuwa zamani.
UMOJA WETU NDIYO UNDUGU WETU...na kijana Wa mwanza
Tuwe na siku iliyonjema kwenu nyoote 🙏🏿🙏🏿