MKUZA GIRLS HIGH SCHool

MKUZA GIRLS HIGH SCHool The school is owned by the Evangelical Lutheran Church in Tanzania – Eastern and Costal Diocese. The school is registered with Reg.no. S. 4900.

It is a school which educates girls from Form 1 – Form 4 in science, arts and commercial combination.

"Tarehe 08/03/2025 ilikuwa siku ya pekee katika shule yetu ya Mkuza Girls Secondary School! Katika kuadhimisha Mkuza Day...
19/03/2025

"Tarehe 08/03/2025 ilikuwa siku ya pekee katika shule yetu ya Mkuza Girls Secondary School! Katika kuadhimisha Mkuza Day, tulijitoa kwa upendo kwa kufanya matendo ya huruma kwa wazee. ❤️ Tumejifunza kuwa maisha ni baraka, na kushiriki na wengine ni njia bora ya kuonyesha shukrani.

Tunaamini kuwa upendo mdogo unaweza kuleta tabasamu kubwa! 😊💙 "

UMUHIMU WA IBADA KWA WANAFUNZI – MKUZA GIRLS SECONDARY SCHOOLIbada ni sehemu muhimu katika maisha ya kila mwanafunzi kwa...
18/03/2025

UMUHIMU WA IBADA KWA WANAFUNZI – MKUZA GIRLS SECONDARY SCHOOL

Ibada ni sehemu muhimu katika maisha ya kila mwanafunzi kwani husaidia katika ukuaji wa kiroho, maadili, na nidhamu. Katika shule ya Mkuza Girls Secondary School, ibada ina nafasi kubwa katika kuimarisha tabia njema na kujenga misingi imara ya maisha. Zifuatazo ni sababu kuu zinazoonyesha umuhimu wa ibada kwa wanafunzi:

1. Kukuza Maadili na Nidhamu

Ibada inawafundisha wanafunzi maadili mema k**a vile unyenyekevu, uaminifu, na heshima kwa wengine. Kupitia mafunzo ya kidini, wanafunzi wanajifunza kuwa waadilifu na kuepuka vitendo vibaya k**a uongo, wizi, na uvivu.

2. Kuimarisha Uhusiano na Mungu

Ibada inawapa wanafunzi nafasi ya kuwasiliana na Mungu kwa sala na nyimbo za ibada. Hii huwasaidia kujenga imani imara na kutegemea msaada wa Mungu katika maisha yao ya kila siku, hasa wanapokabiliana na changamoto za masomo na maisha kwa ujumla.

3. Kusaidia Kukabiliana na Changamoto

Mwanafunzi anapokumbana na matatizo k**a vile msongo wa mawazo, shinikizo la marafiki, au matatizo ya kifamilia, ibada hutoa faraja na tumaini. Inawasaidia kuelewa kuwa Mungu yupo pamoja nao na ana mpango mzuri kwa maisha yao.

4. Kujenga Umoja na Mshik**ano

Ibada huwaleta wanafunzi pamoja k**a jamii moja yenye mshik**ano. Wakati wa ibada, wanafunzi hujifunza kushirikiana, kusameheana, na kusaidiana, hivyo kuimarisha upendo na umoja ndani ya shule.

5. Kuongeza Umakini katika Masomo

Wanafunzi wanaoshiriki ibada mara kwa mara huwa na utulivu wa akili, jambo linalowawezesha kuelewa masomo kwa urahisi. Pia, wanajifunza kuwa wavumilivu na wenye nidhamu, sifa zinazowasaidia kuwa na ufanisi katika taaluma zao.

6. Kutoa Mwongozo wa Maisha

Kupitia ibada, wanafunzi hujifunza mafunzo muhimu ya maisha yanayowasaidia kufanya maamuzi sahihi. Mafundisho ya kiroho huwapa mwanga wa kutofautisha mema na mabaya, hivyo kuwaepusha na mienendo mibaya inayoweza kuathiri mustakabali wao.

NIDHAMU NA TAALUMA: NGUZO YA MAFANIKIOKatika Shule ya Sekondari ya Wasichana Mkuza, tunaamini kuwa nidhamu na taaluma nz...
14/03/2025

NIDHAMU NA TAALUMA: NGUZO YA MAFANIKIO

Katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Mkuza, tunaamini kuwa nidhamu na taaluma nzuri ni misingi imara ya mafanikio. Nidhamu hujenga tabia njema, uwajibikaji, na heshima kwa mwalimu, mwanafunzi, na jamii kwa ujumla. Taaluma bora huleta maarifa, ubunifu, na uwezo wa kushindana katika nyanja mbalimbali za maisha.

Tunajivunia kuwa shule inayokuza maadili mema, bidii katika masomo, na mshik**ano miongoni mwa wanafunzi na walimu. Kwa pamoja, tunajenga kizazi chenye uwezo wa kubadilisha jamii na kuleta maendeleo.

“Elimu bila nidhamu haina maana, na nidhamu bila elimu haina mwelekeo. Tukizingatia vyote viwili, hakuna linaloshindikana!”

Habari njema!Uongozi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Mkuza una furaha kubwa kukualika wewe, mzazi, mdau wa elimu, pam...
08/03/2025

Habari njema!

Uongozi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Mkuza una furaha kubwa kukualika wewe, mzazi, mdau wa elimu, pamoja na wahitimu wote wa shule yetu, kushiriki katika siku maalum ya Mkuza Day, itakayofanyika tarehe 8 Machi 2025 katika Kanisa la KKKT Mkuza.

Siku hii itaambatana na matendo ya huruma kwa wahitaji, kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 3:30 asubuhi, yakifuatiwa na ibada ya shukrani kuanzia saa 4:00 asubuhi katika Kanisa la KKKT Mkuza.

Tunatarajia kushiriki pamoja katika siku hii adhimu. Karibuni nyote!

Habari njema!Uongozi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Mkuza una furaha kubwa kukualika wewe, mzazi, mdau wa elimu, pam...
05/03/2025

Habari njema!

Uongozi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Mkuza una furaha kubwa kukualika wewe, mzazi, mdau wa elimu, pamoja na wahitimu wote wa shule yetu, kushiriki katika siku maalum ya Mkuza Day, itakayofanyika tarehe 8 March 2025 katika Kanisa la KKKT Mkuza.

Siku hii itaambatana na matendo ya huruma kwa wahitaji, kuanzia saa 1:00 asubuhi hadi saa 3:30 asubuhi, yakifuatiwa na ibada ya shukrani kuanzia saa 4:00 asubuhi katika Kanisa la KKKT Mkuza.

Tunatarajia kushiriki pamoja katika siku hii adhimu. Karibuni nyote!

Neno la Shukrani kwa Wazazi, Waalimu na Wanafunzi wa Kidato cha Nne 2024 - Mkuza Girls Secondary SchoolNapenda kutoa shu...
14/02/2025

Neno la Shukrani kwa Wazazi, Waalimu na Wanafunzi wa Kidato cha Nne 2024 - Mkuza Girls Secondary School

Napenda kutoa shukrani za dhati kwa wazazi wa wanafunzi wa Kidato cha Nne 2024, kwa ushirikiano wao na juhudi zao katika kuhakikisha kwamba watoto wao wanapata elimu bora. Mshik**ano wenu na msaada wenu umekuwa ni nguzo kubwa katika mafanikio haya.

Pia, shukrani maalum ziende kwa waalimu wetu kwa kujitolea kwa moyo mmoja katika kufundisha na kuhamasisha wanafunzi wetu. Uongozi wenu bora na bidii yenu katika kuwalea vijana hawa imezaa matunda.

Kwa wanafunzi wa Kidato cha Nne 2024, tunawapongeza kwa juhudi zenu na mafanikio makubwa mlioyapata katika mtihani wa Taifa. Tumefurahi kuona matokeo ya mtihani yakionyesha ufaulu mzuri, ambapo:

Division One: 11

Division Two: 23

Division Three: 9

Division Four: 1

Hii ni ishara ya kazi nzuri iliyofanyika na umoja wa pamoja katika shule yetu. Tunaamini matokeo haya yatakuwa ni chachu ya kuendelea na juhudi katika masomo yenu ya baadaye.

Tunamshukuru Mungu kwa kutuwezesha kufikia hatua hii. Tunaendelea kumtumainia Mungu kwa mafanikio zaidi katika mwaka ujao.

Kwa niaba ya uongozi wa shule, nawashukuru tena kwa kazi kubwa mliofanya. Mungu awabariki na awajalie mafanikio zaidi.

Mkuu wa Shule
Mkuza Girls Secondary School

NENO LA SHUKRANI kwa Wanafunzi, Waalimu, Watumishi Wasio Waalimu na Wazazi wa Shule ya Mkuza Girls Secondary School kwa ...
09/01/2025

NENO LA SHUKRANI kwa Wanafunzi, Waalimu, Watumishi Wasio Waalimu na Wazazi wa Shule ya Mkuza Girls Secondary School kwa Kufanya Vema Katika Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Pili 2024

Nashukuru kwa niaba ya uongozi wa shule ya Mkuza Girls Secondary School, kwa niaba ya wanafunzi wetu wa kidato cha pili, waalimu, watumishi wasio waalimu na wazazi wote, kwa mafanikio makubwa tuliyoyapata katika mtihani wa taifa wa kidato cha ii 2024

Mafanikio haya ni matokeo ya juhudi na ushirikiano wa dhati kati ya wanafunzi wetu, walimu wetu wa kujitolea, watumishi wetu wasio waalimu ambao wanatoa msaada mkubwa kila siku, na wazazi ambao wamekuwa bega kwa bega na sisi kuhakikisha wanafunzi wetu wanapata elimu bora. Ni kutokana na kujituma kwetu sote, kuzingatia masomo kwa bidii na kujitolea kwa dhati, kwamba tumefanikisha hili.

Tunatambua kuwa mafanikio haya hayakuja kirahisi, bali ni matokeo ya kila mmoja wetu kujitolea kwa kiwango cha juu na kufanya kazi kwa umoja na malengo ya pamoja. Wanafunzi wetu wameonyesha juhudi kubwa katika kujifunza na kuboresha ufanisi wao. Walimu wameendelea kutoa elimu bora na kusaidia wanafunzi kufikia malengo yao. Watumishi wasio waalimu wamekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha mazingira ya shule yanabaki salama na yanayofaa kwa wanafunzi kujifunza. Wazazi wamesaidia kwa namna mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kutoa ushirikiano na rasilimali zinazohitajika kwa maendeleo ya watoto wao.

Ningependa kuwasihi wanafunzi wetu wa kidato cha pili waendelee kujitahidi na kufanya vizuri zaidi katika masomo yao, kwani mafanikio haya ni mwanzo wa safari ndefu na yenye changamoto, lakini pia fursa kubwa. Aidha, niwapongeze tena waalimu na watumishi wote kwa juhudi zao zisizo na kifani na kuendelea kuwa msaada mkubwa katika maendeleo ya elimu ya shule hii.

Kwa wazazi, tunawashukuru kwa kuendelea kuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya watoto wenu. Ushirikiano wenu na shule ni wa thamani kubwa na tunatambua mchango wenu katika kufanikisha lengo hili.
Hongera kwa kila mmoja wenu, na nawaahidi kuwa tutendelea kuweka juhudi katika kukuza vipaji na maarifa ya wanafunzi wetu, kuhakikisha kuwa wanapata elimu bora na kuwa sehemu ya mafanikio ya kitaifa.

MKUU WA SHULE.

25/12/2024
Picha za matukio ya ziara za kimasomo zikionesha Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Mkuza wakijifunza na kufur...
09/12/2024

Picha za matukio ya ziara za kimasomo zikionesha Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Mkuza wakijifunza na kufurahia uhifadhi wa Mazingira.







Huu ni ushuhudawa mwanafunzi aliye wahi kusoma shuleni kwetu
18/11/2024

Huu ni ushuhudawa mwanafunzi aliye wahi kusoma shuleni kwetu

Address

P. O BOX 30882
Kibaha

Opening Hours

Monday 07:00 - 17:00
Tuesday 07:00 - 17:00
Wednesday 07:00 - 17:00
Thursday 07:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 07:00 - 17:00
Sunday 07:00 - 17:00

Telephone

+255754631635

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MKUZA GIRLS HIGH SCHool posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The School

Send a message to MKUZA GIRLS HIGH SCHool:

Shortcuts

Share

Category