Elimu sahihi ya Uislamu

Elimu sahihi ya Uislamu العلم نور،فنظر عمن اتخذ دينك!

09/07/2026

Surat aarafu.

Assalaamu alaykum warahmatullahi wabarakatuhu.Sifa zote njema ni za Allah na rehma na amani zimuendee mtume wetu Muhamma...
25/06/2026

Assalaamu alaykum warahmatullahi wabarakatuhu.
Sifa zote njema ni za Allah na rehma na amani zimuendee mtume wetu Muhammad ﷺ na aali zake na maswahaba wake

Baada ya hayo :

Waislamu : Laa Takuunu Imma’a Msifuate Watu Bila Elimu yaani msiwe bendera fuata upepo.

Kwa jina la Allah, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.

Katika maisha ya mwanadamu, mojawapo ya mitihani mikubwa si tu kujua lililo haki, bali kuweza kusimama juu ya haki hiyo hata pale watu wengi wanapokwenda kinyume nayo. Ndiyo maana Mtume ﷺ alitufundisha msingi wa hekima kubwa aliposema:

👉Laa takuunu imma’a…
Msijifanye wafuasi ovyo (kufuata kila mtu bila kufikiri).

Leo natoa nasaha ambazo zinayomlinda muislamu dhidi ya kupotea kwa sababu ya wingi wa watu au mvuto wa jamii.

EWE MUISLAMU, mfuasi wa mtume :

1. Haki haipimwi kwa watu bali watu hupimwa kwa haki

Hekima kubwa iliyonukuliwa kutoka kwa Ali ibn Abi Talib inasema:

👉Inna al-haqqa wal-baatila laa yu’rafaani bi aqdaari ar-rijaal…

Haki na batili hazitambuliki kwa hadhi ya watu.”

Kisha akaendelea kusema:
I’rifil haqqa ta’rif ahlahu, wa i’rifil baatila ta’rif ahlahu.

Itambue haki, ndipo utawajua watu wake; na itambue batili, ndipo utawajua watu wake.

Hapa tuna fundisho kubwa:
Usimfuate mtu halafu ukadhani kila analosema ni haki. Bali chukua haki yenyewe, kisha angalia nani anaiwafuata.

2. Qur’an inatahadharisha kufuata wengi bila uhakika

Allah anasema:
Na ukiwatii wengi wa waliomo duniani watakupoteza njia ya Mwenyezi Mungu. (Al-An’am 6:116)

Hii inaonyesha kuwa:

Wingi wa watu hauhalalishi jambo kuwa la haki
Wengi wanaweza kuwa kwenye upotofu

3. Mtume ﷺ alikataza kufuata bila kufikiri

Mtume ﷺ pia alionya dhidi ya kuwa mfuasi kipofu:

👉Msijifanye imma’a; mnasema tukiwa watu wema tutakuwa wema, na wakifanya uovu tutafanya uovu.

Hii ni elimu ya tabia:
Usikubali kubebwa na mkondo wa watu
Fikiria kabla ya kufuata

4. Haki ina dalili, si umaarufu

Katika msingi wa Uislamu, haki haijengwi kwa hisia bali kwa dalili. Mtume ﷺ amesema:

Al-haqqu ma‘ahu dalil.
Haki ina dalili yake.

Hapa tunaona:

Sio kila linalosemwa kwa nguvu ni haki
Sio kila linalokubaliwa na wengi ni sahihi
Bali haki ina ushahidi wake

5. Wanazuoni waliweka msingi wa kutofuata mtu bila dalili

👉Imam Malik رحمه الله alisema:
“Kila mtu anaweza kukubaliwa na kukataliwa, isipokuwa Mtume ﷺ.”

👉Na Imam Shafi’i رحمه الله akasema:
“Ukiona kauli yangu inapingana na hadithi sahihi, ipuuzie kauli yangu.”

👉Na Imam Ahmad ibn Hanbal رحمه الله akasisitiza:
“Msifuate mimi wala Malik wala Shafi’i, chukueni kutoka pale walipotoka (Qur’an na Sunnah).”

👉👉Hawa wote wanakupa msingi mmoja: Mtu hafuatwi kwa ubinafsi wake, bali kwa ukweli alioubeba.

6. Muunganiko wa hekima zote

Ukiziunganisha kauli hizi zote, tunapata picha moja ya elimu:

Haki haitegemei watu
Haki haitegemei wingi
Haki haitegemei hadhi
Haki haitegemei msisimko wa jamii

Bali:

Haki hujulikana kwa dalili
Haki hujulikana kwa Qur’an na Sunnah
Haki hujulikana kwa uadilifu wake wenyewe

Kwa kumaliza , chukua haya maneno ya Imamu Auzaa'iyyu Allah amrehemu
Yatakusaidia

Anasema :

اصبر نفسك على السنة، وقف حيث وقف القوم، وقل بما قالوا، وكف عما كفوا عنه، واسلك سبيل سلفك الصالح، فإنه يسعك ما وسعهم.
Tafsiri yake:
"Jilazimishe kushik**ana na Sunnah. Simama pale waliposimama watu (wema waliotangulia). Sema waliyoyasema. Jizuie na yale waliyojizuia nayo. Fuata njia ya Salafu wema; kwani kilichowatosha wao kitakutosha na wewe."

Anasema pia Imamu Auzaa'iyyu (Allah amrehemu)
عليك بآثار من سلف وإن رفضك الناس، وإياك وآراء الرجال وإن زخرفوها لك بالقول، فإن الأمر ينجلي وأنت على طريق مستقيم.

Maana yake:
"Shik**ana na athari (njia) za waliotangulia, hata k**a watu watakukataa. Jihadhari na maoni ya watu, hata wakiyakupamba kwa maneno mazuri. Hakika mwisho wa mambo utadhihirika, na utakuwa uko juu ya njia iliyonyooka."

👉 Huu ni ukurasa unaofundisha Uislamu sahihi bila kueneza chuki baina ya waislamu.

MAWAIDHA: SUBIRA NI NGAO BORA YA KUPAMBANA NA MITIHANI Ndugu zangu katika Imani,Maisha ya dunia si makazi ya starehe ya ...
19/06/2026

MAWAIDHA: SUBIRA NI NGAO BORA YA KUPAMBANA NA MITIHANI

Ndugu zangu katika Imani,

Maisha ya dunia si makazi ya starehe ya kudumu, bali ni uwanja wa mitihani. Kila mwanadamu anayekanyaga ardhi hii atakutana na aina mbalimbali za majaribu; wengine hujaribiwa kwa umasikini, wengine kwa utajiri, wengine kwa maradhi, wengine kwa huzuni, na wengine kwa kupoteza wapendwa wao.

Lakini Uislamu umetufundisha namna bora ya kukabiliana na changamoto hizi zote. Dawa kubwa ambayo Allah ametuwekea ni Subira.

Subira ni uwezo wa moyo kubaki thabiti, ulimi kubaki na maneno mema, na viungo kubaki katika utiifu wa Allah wakati wa mitihani na misukosuko.

Allah (Subhānahu wa Ta‘ālā) anasema:

﴿ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اصْبِرُوا وَصَابِرُوا وَرَابِطُوا وَاتَّقُوا اللَّهَ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ ﴾ (Āl ‘Imrān: 200)

Hivyo basi, hali yoyote uliyonayo leo, fahamu kwamba mitihani ni sehemu ya maisha. Uwe tajiri au maskini, muumini au kafiri, hakuna anayeishi duniani bila kuonja majaribu.

Ndiyo maana Mtume ﷺ amesema:

«عَجَبًا لِأَمْرِ الْمُؤْمِنِ، إِنَّ أَمْرَهُ كُلَّهُ خَيْرٌ، وَلَيْسَ ذَاكَ لِأَحَدٍ إِلَّا لِلْمُؤْمِنِ، إِنْ أَصَابَتْهُ سَرَّاءُ شَكَرَ فَكَانَ خَيْرًا لَهُ، وَإِنْ أَصَابَتْهُ ضَرَّاءُ صَبَرَ فَكَانَ خَيْرًا لَهُ»

Ndugu zangu,

Allah ametupa ngao mbili za kutusaidia kupambana na shida na mitihani:

﴿ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَعِينُوا بِالصَّبْرِ وَالصَّلَاةِ ۚ إِنَّ اللَّهَ مَعَ الصَّابِرِينَ ﴾ (Al-Baqarah: 153)

Hivyo, silaha ya muumini si kulalamika, bali ni kuswali na kusubiri msaada wa Allah kwa subira.

Fahamuni pia kuwa mwanadamu hakuumbwa ili aishi maisha ya raha bila mitihani.

Allah anasema:

﴿ أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَن يُتْرَكَ سُدًى ﴾ (Al-Qiyāmah: 36)

Na amesema:

﴿ إِنَّا خَلَقْنَا الْإِنسَانَ مِن نُّطْفَةٍ أَمْشَاجٍ نَّبْتَلِيهِ فَجَعَلْنَاهُ سَمِيعًا بَصِيرًا ﴾ (Al-Insān: 2)

Kwa nini Allah anatupa mitihani?

1. Kwa sababu anawapenda baadhi ya waja Wake

Mtume ﷺ amesema:

«إِنَّ عِظَمَ الْجَزَاءِ مَعَ عِظَمِ الْبَلَاءِ، وَإِنَّ اللَّهَ إِذَا أَحَبَّ قَوْمًا ابْتَلَاهُمْ»

Hivyo si kila mtihani ni adhabu. Wakati mwingine ni ishara ya mapenzi ya Allah kwa mja Wake.

2. Mitihani ni kipimo cha Imani

Mtume ﷺ amesema:

«يُبْتَلَى الرَّجُلُ عَلَى قَدْرِ دِينِهِ، فَإِنْ كَانَ فِي دِينِهِ صَلَابَةٌ زِيدَ فِي بَلَائِهِ»

Na katika hadithi nyingine amesema:

«أَشَدُّ النَّاسِ بَلَاءً الْأَنْبِيَاءُ، ثُمَّ الْأَمْثَلُ فَالْأَمْثَلُ»

Ndiyo maana Manabii walipitia majaribu makubwa sana. Nabii Nūh, Nabii Ibrāhīm, Nabii Mūsā, Nabii Ayyūb na Manabii wengine wote walijaribiwa. Hata Mtume wetu Muhammad ﷺ alipitia mitihani mingi.

Allah akamwambia:

﴿ فَصَبْرٌ جَمِيلٌ ﴾

Na akasema:

﴿ فَاصْبِرْ كَمَا صَبَرَ أُولُو الْعَزْمِ مِنَ الرُّسُلِ ﴾

Na akasema:

﴿ وَاصْبِرْ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ ﴾

3. Mitihani ni mtihani wa matendo yetu

Hapa ndipo jibu kuu la kwa nini Allah anatupa mitihani linapatikana.

Allah amesema:

﴿ الَّذِي خَلَقَ الْمَوْتَ وَالْحَيَاةَ لِيَبْلُوَكُمْ أَيُّكُمْ أَحْسَنُ عَمَلًا ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْغَفُورُ ﴾ (Al-Mulk: 2)

Faida za Subira

1. Kusamehewa madhambi

Mtume ﷺ amesema:

«مَا يُصِيبُ الْمُسْلِمَ مِنْ نَصَبٍ وَلَا وَصَبٍ وَلَا هَمٍّ وَلَا حُزْنٍ وَلَا أَذًى وَلَا غَمٍّ حَتَّى الشَّوْكَةِ يُشَاكُهَا إِلَّا كَفَّرَ اللَّهُ بِهَا مِنْ خَطَايَاهُ»

Kila maumivu, huzuni, uchovu na hata mwiba unaomchoma muumini huwa sababu ya kufutiwa baadhi ya madhambi yake.

2. Kupata rehema na baraka za Allah

Allah amesema:

﴿ وَلَنَبْلُوَنَّكُم بِشَيْءٍ مِّنَ الْخَوْفِ وَالْجُوعِ وَنَقْصٍ مِّنَ الْأَمْوَالِ وَالْأَنفُسِ وَالثَّمَرَاتِ ۗ وَبَشِّرِ الصَّابِرِينَ ۝ الَّذِينَ إِذَا أَصَابَتْهُم مُّصِيبَةٌ قَالُوا إِنَّا لِلَّهِ وَإِنَّا إِلَيْهِ رَاجِعُونَ ۝ أُولَٰئِكَ عَلَيْهِمْ صَلَوَاتٌ مِّن رَّبِّهِمْ وَرَحْمَةٌ ۖ وَأُولَٰئِكَ هُمُ الْمُهْتَدُونَ ﴾ (Al-Baqarah: 155–157)

3. Kupata malipo yasiyo na hesabu

Allah amesema:

﴿ إِنَّمَا يُوَفَّى الصَّابِرُونَ أَجْرَهُم بِغَيْرِ حِسَابٍ ﴾ (Az-Zumar: 10)

Subira ndiyo ibada ambayo Allah ameahidi kuilipa bila hesabu maalumu.

Wale wote wenye shida za maisha, mitihani mbalimbali, taabu za kimaisha...sikilizeni haya maneno:

يا صاحبَ الهمِّ إنَّ الهمَّ مُنفرجٌ
أبشرْ بخيرٍ فإنَّ الفارجَ اللهُ

Ewe mwenye huzuni, hakika huzuni itaondoka.
Furahia habari njema, kwani Mwenye kuondoa dhiki ni Allah.

اليأسُ يقطعُ أحيانًا بصاحبِهِ
لا تيأسنَّ فإنَّ الكافيَ اللهُ

Kukata tamaa humwangamiza mtu wakati mwingine.
Usikate tamaa, kwani Mwenye kutosha kwa kila jambo ni Allah.

اللهُ يُحدِثُ بعدَ العُسرِ ميسرةً
لا تجزعنَّ فإنَّ القاسمَ اللهُ

Allah huleta wepesi baada ya ugumu.
Usihuzunike, kwani Mgawaji wa riziki na neema zote ni Allah.

إذا بُلِيتَ فثقْ باللهِ وارضَ بهِ
إنَّ الذي يكشفُ البلوى هو اللهُ

Unapopatwa na mtihani, mtumainie Allah na ridhika na hukumu Yake.
Hakika Anayeondoa matatizo na misiba ni Allah.

إذا قضى اللهُ فاستسلِمْ لقدرتهِ
ما لامرئٍ حيلةٌ فيما قضى اللهُ

Allah anapokadiria jambo, salimu amri kwa uwezo Wake.
Hakuna mwanadamu mwenye ujanja mbele ya alichokikadiria Allah.

واللهِ ما لكَ غيرُ اللهِ من أحدٍ
فحسبُكَ اللهُ في كلٍّ لكَ اللهُ

Naapa kwa Allah, huna mlinzi mwingine isipokuwa Allah.
Basi Allah Anakutosha katika kila jambo; Allah yuko pamoja nawe.

اللهُ حسبُكَ ممَّا عذتَ منهُ بهِ
وأينَ يُمنَعُ مَن كانتْ لهُ اللهُ

Allah Anakutosha dhidi ya kila jambo uliloomba ulinzi Kwake.
Na ni nani awezaye kuzuiliwa ilhali Allah ndiye Mlinzi wake?

يا نفسُ صبرًا على ما قدَّرَ اللهُ
وسلِّمي تسلمي فالحاكمُ اللهُ

Ewe nafsi yangu, vumilia yale aliyoyakadiria Allah.
Na salimu amri, utasalimika; kwani Hakimu wa kweli ni Allah.

يا ربَّ مستصعبٍ قد سهَّلَ اللهُ
وربَّ شرٍّ كثيرٍ قد وقى اللهُ

Ni mambo mangapi yaliyokuwa magumu, kisha Allah akayarahisisha.
Na ni maovu mangapi makubwa, ambayo Allah ameyakinga na kuyaepusha.

K**A BAADO HUJAFOLLOW : TU FOLLOW

Hii ndio ratiba ya masomo na inshallah inaanza kesho Jumatatu → AqidaJumanne → HadithiJumatano → FiqhiAlhamisi → SiraIju...
17/06/2026

Hii ndio ratiba ya masomo na inshallah inaanza kesho

Jumatatu → Aqida
Jumanne → Hadithi
Jumatano → Fiqhi
Alhamisi → Sira
Ijumaa → Khutba/Nasaha
Jumamosi → Maswali na Majibu +mawaidha ya kawaida
Jumapili → Kumbusho la Kiislamu (Shorts/Reels)

Karibu kwenye page yetu ewe muislamu

الذُّنُوبُ الْعَشْرَةُ الْكَبِيرَةُ فِي الإِسْلَامِ الَّتِي يَجِبُ الاجْتِنَابُ عَنْهَاهناك ذنوب لا تُفسد حياة الإنسان ف...
08/05/2026

الذُّنُوبُ الْعَشْرَةُ الْكَبِيرَةُ فِي الإِسْلَامِ الَّتِي يَجِبُ الاجْتِنَابُ عَنْهَا

هناك ذنوب لا تُفسد حياة الإنسان في الدنيا فحسب…
بل قد تُهلك آخرتَه إن لم يتب منها توبةً صادقة.

والأشدُّ حُزنًا أن بعض هذه الذنوب أصبح يُنظر إليها اليوم وكأنها أمور عادية في المجتمع.

وفي الإسلام ليست الذنوب سواء؛
فهناك صغائر، وهناك كبائر لها آثار عظيمة في الدنيا والآخرة.

1. الشِّرْكُ بِاللَّهِ

قال الله تعالى:

﴿إِنَّ اللَّهَ لَا يَغْفِرُ أَنْ يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَنْ يَشَاءُ ۚ وَمَنْ يُشْرِكْ بِاللَّهِ فَقَدِ افْتَرَىٰ إِثْمًا عَظِيمًا﴾
[النساء: 48]

الفائدة:
الشرك أعظم الذنوب عند الله تعالى.

2. قَتْلُ النَّفْسِ بِغَيْرِ حَقٍّ

قال الله تعالى:

﴿وَمَنْ يَقْتُلْ مُؤْمِنًا مُتَعَمِّدًا فَجَزَاؤُهُ جَهَنَّمُ خَالِدًا فِيهَا…﴾
[النساء: 93]

الفائدة:
حياة الإنسان عظيمةٌ ومقدسة عند الله.

3. تَرْكُ الصَّلَاةِ تَعَمُّدًا

قال الله تعالى:

﴿فَوَيْلٌ لِلْمُصَلِّينَ ۝ الَّذِينَ هُمْ عَنْ صَلَاتِهِمْ سَاهُونَ﴾
[الماعون: 4-5]

الفائدة:
الصلاة عماد الدين، وهي الصلة المباشرة بين العبد وربه.

4. عُقُوقُ الْوَالِدَيْنِ

قال الله تعالى:

﴿وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا…﴾
[الإسراء: 23]

الفائدة:
للوالدين منزلة عظيمة في الإسلام.

5. الزِّنَا

قال الله تعالى:

﴿وَلَا تَقْرَبُوا الزِّنَا ۖ إِنَّهُ كَانَ فَاحِشَةً وَسَاءَ سَبِيلًا﴾
[الإسراء: 32]

الفائدة:
الإسلام لم يُحرِّم الزنا فقط، بل حرَّم كل الطرق المؤدية إليه.

6. الرِّبَا

قال الله تعالى:

﴿وَأَحَلَّ اللَّهُ الْبَيْعَ وَحَرَّمَ الرِّبَا﴾
[البقرة: 275]

الفائدة:
الرِّبا يمحق البركة من المال.

7. الْخَمْرُ وَالْمُسْكِرَاتُ

قال الله تعالى:

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنْصَابُ وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ مِنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ…﴾
[المائدة: 90]

وقال النبي ﷺ:

«كُلُّ مُسْكِرٍ حَرَامٌ»
[رواه مسلم]

8. السَّرِقَةُ وَالْغِشُّ

قال الله تعالى:

﴿وَالسَّارِقُ وَالسَّارِقَةُ فَاقْطَعُوا أَيْدِيَهُمَا…﴾
[المائدة: 38]

الفائدة:
الأمانة أساس استقامة المجتمع.

9. شَهَادَةُ الزُّورِ

قال الله تعالى:

﴿وَاجْتَنِبُوا قَوْلَ الزُّورِ﴾
[الحج: 30]

وقال النبي ﷺ:

«أَلَا أُنَبِّئُكُمْ بِأَكْبَرِ الْكَبَائِرِ؟ … وَشَهَادَةُ الزُّورِ»
[متفق عليه]

10. الْكِبْرُ وَالتَّكَـبُّرُ

قال الله تعالى:

﴿إِنَّ اللَّهَ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخْتَالٍ فَخُورٍ﴾
[لقمان: 18]

وقال النبي ﷺ:

«لَا يَدْخُلُ الْجَنَّةَ مَنْ كَانَ فِي قَلْبِهِ مِثْقَالُ ذَرَّةٍ مِنْ كِبْرٍ»
[رواه مسلم]

حَقِيقَةُ الْحَيَاةِ

إنَّ هذه الذنوب تبدأ صغيرة:
فكرة…
ثم عادة…
ثم صحبة سيئة…
ثم بيئة فاسدة…

ولذلك ينبغي للمؤمن أن يكون حذرًا في كل يوم.

التَّوْبَةُ وَرَحْمَةُ اللَّهِ

قال الله تعالى:

﴿قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَىٰ أَنْفُسِهِمْ لَا تَقْنَطُوا مِنْ رَحْمَةِ اللَّهِ…﴾
[الزمر: 53]

الفائدة:
لا يوجد ذنب أعظم من رحمة الله إذا تاب العبد بصدق.

تَنْبِيهٌ

لا تستهِن بأي ذنب.
فقد يكون صغيرًا اليوم…
ثم يصبح عظيمًا غدًا إن لم يُتَبْ منه.

14/02/2026

قال أبو ذر رضي الله عنه
أوصاني خليلي ﷺ بسبعٍ:
1️⃣ أوصاني بحبِّ المساكينِ والدنوِّ منهم.
2️⃣ وأوصاني أن أنظرَ إلى من هو دوني، ولا أنظرَ إلى من هو فوقي.
3️⃣ وأوصاني أن أصلَ رحِمي وإن أدبرت.
4️⃣ وأوصاني ألا أسألَ أحدًا شيئًا.
5️⃣ وأوصاني أن أقولَ بالحقِّ وإن كان مُرًّا.
6️⃣ وأوصاني ألا أخافَ في اللهِ لومةَ لائمٍ.
7️⃣ وأوصاني أن أُكثرَ من قولِ: لا حولَ ولا قوةَ إلا بالله، فإنها كنزٌ من كنوزِ الجنة.

1️⃣ "أوصاني بحبِّ المساكينِ والدنوِّ منهم"
الإسلامُ يبني قلبَ الرحمةِ، والتواضعِ، ويزيلُ الكِبر.
حبُّ المساكين ليس شعورًا فقط، بل هو:
✔ احترامُهم
✔ مساعدتُهم
✔ الجلوسُ معهم بلا احتقار

📖 آيات
﴿وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِلْمُؤْمِنِينَ﴾
📚 (سورة الحجر 15:88)
﴿وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ﴾
📚 (سورة الشعراء 26:215)

🕊 حديث
قال رسول الله ﷺ:
«هَلْ تُنْصَرُونَ وَتُرْزَقُونَ إِلَّا بِضُعَفَائِكُمْ؟»
📚 (رواه البخاري)

📖 سورة الإنسان – الآية 8
﴿وَيُطْعِمُونَ الطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِ مِسْكِينًا وَيَتِيمًا وَأَسِيرًا﴾

2️⃣ "أن أنظرَ إلى من هو دوني ولا أنظرَ إلى من هو فوقي"
في أمور الدنيا:
النظرُ إلى من هو فوقك → حزنٌ وحسد
النظرُ إلى من هو دونك → شكرٌ ورضا

🕊 حديث
«انْظُرُوا إِلَى مَنْ هُوَ أَسْفَلَ مِنْكُمْ، وَلَا تَنْظُرُوا إِلَى مَنْ هُوَ فَوْقَكُمْ، فَهُوَ أَجْدَرُ أَلَّا تَزْدَرُوا نِعْمَةَ اللَّهِ عَلَيْكُمْ»
📚 (رواه مسلم)

📖 آية
﴿لِكَيْلَا تَأْسَوْا عَلَىٰ مَا فَاتَكُمْ﴾
📚 (سورة الحديد 57:23)

3️⃣ "أن أصل رحمي وإن أدبرت"
صلةُ الرحمِ من أعظمِ ما أكَّد عليه الإسلام.
📖 آية
﴿وَاتَّقُوا اللَّهَ الَّذِي تَسَاءَلُونَ بِهِ وَالْأَرْحَامَ﴾
📚 (سورة النساء 4:1)

🕊 أحاديث
قال رسول الله ﷺ:
«مَنْ سَرَّهُ أَنْ يُبْسَطَ لَهُ فِي رِزْقِهِ، وَيُنْسَأَ لَهُ فِي أَثَرِهِ، فَلْيَصِلْ رَحِمَهُ»
📚 (رواه البخاري ومسلم)

وقال ﷺ:
«لَا يَدْخُلُ الْجَنَّةَ قَاطِعُ رَحِمٍ»
📚 (رواه البخاري ومسلم)
4️⃣ "ألا أسأل أحدًا شيئًا"

ثمراتُه:
✔ بناءُ الكرامةِ
✔ التوكلُ على الله
✔ اجتنابُ ذلِّ السؤال
📖 آية
﴿وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَارْغَبْ﴾

📚 (سورة الشرح 94:8)
🕊 أحاديث
«وَمَنْ يَسْتَعْفِفْ يُعِفَّهُ اللَّهُ»
📚 (رواه البخاري ومسلم)

عن عبد الله بن عمر رضي الله عنهما قال:
قال رسول الله ﷺ:
«مَا يَزَالُ الرَّجُلُ يَسْأَلُ النَّاسَ حَتَّى يَأْتِيَ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَلَيْسَ فِي وَجْهِهِ مُزْعَةُ لَحْمٍ»

وقال ﷺ:
«مَنْ سَأَلَ النَّاسَ أَمْوَالَهُمْ تَكَثُّرًا، فَإِنَّمَا يَسْأَلُ جَمْرًا، فَلْيَسْتَقِلَّ أَوْ لِيَسْتَكْثِرْ»

5️⃣ "أن أقول بالحق وإن كان مرًّا"
📖 آية
﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُونُوا قَوَّامِينَ بِالْقِسْطِ﴾
📚 (سورة النساء 4:135)
🕊 حديث
«أَفْضَلُ الْجِهَادِ كَلِمَةُ حَقٍّ عِنْدَ سُلْطَانٍ جَائِرٍ»
📖 سورة الأحزاب – الآية 70
﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ وَقُولُوا قَوْلًا سَدِيدًا﴾
🕊 حديث
«مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ فَلْيَقُلْ خَيْرًا أَوْ لِيَصْمُتْ»
📚 (رواه البخاري ومسلم)

11/02/2026

Ramadhani is coming soon
Be prepared

15/01/2026

Page hii itafundisha Fiqhi,aqida,Sira,hadithi swahihi zilizothibiti

15/01/2026

Assalaamu alaykum warahmatullahi wabarakatuhu
Kwanzia Leo Kuwa karibu na page hii
Elimu ya dini ya Uislamu itapostiwa Kila siku

07/09/2025

أدب النوم 😑😑

Address

Tanzania
Geita

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Elimu sahihi ya Uislamu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category