23/05/2026
Mpira unaenda Kasi tofauti na ww unaepata nafasi ya kuutazama kwenye video ya marudio
Goli kipa anauona kwa mara moja tu Mpira ukiwa ushafika golini ukiwa na Kasi
Magoli hayo wamefungwa makipa wengi tu na huwa hawaruki wanabaki wamesimama tu
Nenda katazame marudio ya mechi ya Astonvilla vs Man U anafungwa Same Lames hakujishughulisha kabisa amefungwa Donnaruma na Bournemouth hakujishughulisha kabisa nyinyi mnataka mtu aonyeshe reaction ya kufuata Mpira wakati ushampita si kichekesho hicho
Mpira aliyepiga Okello ni K**a Kuna deflection au mzungusho nyuma ya ukuta ambao pia ulipoteza uelekeo wa Mpira na kumuadaa goli kipa
Tatizo mnauchukulia Mpira K**a mnavoutazama kwenye tv au kuhadithiana vijiweni ila K**a umecheza Mpira hata Chandimu tu utaelewa Kuna mipira ukiuzwa husumbuki unaganda K**a Sanamu
Aziz K aliwafunga mabao ya kudundisha Mpira watu wakaona K**a makipa wamepangwa alivoanza kuwafunga na wa kimataifa ndo watu wakaelewa
Mpira ni mchezo wa wazi tuache siasa
K**a wamefix mechi labda upande wa wachezaji wa ndani lakini hakuna goli la kumlaumu kipa hapo
Msiendeshwe na ushabiki wa kipumbavu mnamchafua goli kipa Ile ni kazi yake
Wachezaji wanajitoa maisha yao kutuburudisha ila sisi tunawavunja moyo tunawaumiza tunawaharibia mkate wao hususani hawa wazawa
Angefungwa DIARA au KASARI tungekaa kimya