22/07/2026
*Hesabu 23:1-2,6-8,11-12*
[1]Balaamu akamwambia Balaki, Nijengee hapa madhabahu saba, ukaniandalie hapa ngโombe waume saba, na kondoo waume saba.
[2]Balaki akafanya k**a Balaamu alivyonena. Balaki na Balaamu wakatoa sadaka, ngโombe mume mmoja na kondoo mume mmoja juu ya kila madhabahu.
[6]Akarudi kwake, na tazama, amesimama karibu na sadaka yake ya kuteketezwa, yeye na wakuu wote wa Moabu pamoja naye.
[7]Akatunga mithali yake, akasema, Balaki amenileta kutoka Aramu,
Mfalme wa Moabu kutoka milima ya mashariki,
Njoo! Unilaanie Yakobo,
Njoo! Unishutumie Israeli.
[8]Nimlaanije, yeye ambaye Mungu hakumlaani?
Nimshutumuje, yeye ambaye BWANA hakumshutumu?
[11]Balaki akamwambia Balaamu, Umenitendea nini? Nimekuleta ili Uwalaani adui zangu, na tazama, umewabariki kabisa kabisa.
[12]Naye akajibu, akasema, Je! Hainipasi kuangalia, niseme neno lile BWANA atialo kinywani mwangu?
Mpendwa katika maisha yetu yapo mambo yanayotutesa kwa sababu wapo watu waliokwenda katika madhabahu zao za giza wakatulaania magonja, wakatulaania tusifanikiwe na wametoa sadaka kubwa na nyingine nyingi. Lakini sikia hili neno
๐
Isaya 54:17
[17]Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa BWANA, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema BWANA.
๐
*Isaya 7:7*
[7]Bwana MUNGU asema hivi, Neno hili halitasimama wala halitakuwa.
๐
*Zaburi 105:15*
[15]Akisema, Msiwaguse masihi
wangu,
Wala msiwadhuru nabii zangu.
Mpendwa Mungu anatupenda na anatuwazia mema hivyo hatakubali kuona adui akitulaani katika madhabahu zao akanyamaza. Mungu ametutetea bila hata sisi kujua k**a tupo kwenye hatari.
*Nikutakie Jumatano njema Mpendwa Endelea kumwamini na kumtii. Omba bila kuchoka.*