Fikra za Kiswahili

Fikra za Kiswahili Kiswahili nguzo ya umoja wa africa(KINA)

23/01/2026

FIKRA ZA LUGHA YA KISWAHILI

Mwana wa Afrika, panda mbegu zako zenye hekima ya hatima ya lugha ya Kiswahili. Ili kufuata njia na kutimiza maono ya waasisi wa bara letu. Ninazungumza hivi kwa sababu Nimekuwa nikifuatilia mienendo ya tabia na mtazamo wa baadhi naona kubeba upotofu kuhusu lugha ya Kiswahili kwa sababu ya kusumba za kikoloni ambazo zinaishi katika fikra zao. Hali hii ichukulie kwa uzito, kabla ya kizazi kijacho hakijakufikia.
Maana kutafuta mti ulioteuliwa na fikra potofu za kuamini lugha za kigeni ni kulaani afrika wako. Amka! ichunguze na kuifuata njia inayotazamwa na dhamiri ya mama Afrika. Maana hekima nisemayo hutembea mahali penye sauti tulivu iliyobeba hatima tukufu ya mama Afrika. Sio pale penye kelele za hila.
Kumbuka Maisha yanakuwa na maana unapogundua kwamba kila kitu kuwa kizuri unapokiangalia kwa upendo. Unapoanza kuyaona maisha si kwa kile tu yanakupa, bali pia kwa yale yanayotokea katikati, na hata wakati kila kitu kinapobadilika, ndipo unaanza kuelewa uzuri wake.
Kwa hiyo ni wakati ambapo Afrika hatuitaji kupotea katika hofu, shaka au kuwafurahisha wabaya na kuzurura gizani wakati babu zetu na waasisi wa bara letu la Afrika waliandika maono vibaoni ili kila mmoja asome, Pia walishaonyesha njia itakayotufanya kuwa wamoja, njia ambayo ni lugha ya Kiswahili ♥️. Vilevile waliamini kuwa lugha hii ndio itakayowafanya waafrika kupika chakula kizuri na chenye lishe kwa mama Afrika. Sasa ili Afrika ijitukuze na kutumia vipawa na uwezo wake haina budi kutumia lugha ya Kiswahili katika kufanya tafiti na kubuni teknolojia za asili kuanzia vikaushio vya sola, vichujio vya maji, droni za kilimo, hadi zana za afya za kidijitali.
Aidha kupitia umoja wa waafrika, Afrika itazungumza na kufikiri namna ya kubadili hesabu kuwa mashine, dhana kuwa vielelezo na data kuwa maamuzi ili kuondoa utegemezi kutoka nje.
Pia watahitaji kuenda mbali nakufanya TEHAMA kuzungumza lugha ya Kiswahili na kuweza kuunda programu zinazosaidia biashara za ndani, shule, vyuo au hospitali.
Hizi Akili zetu bora zitazungumza na kufikiri kwa kutumia lugha ya Kiswahili zitajikita katika kujenga viwanda, mfano kutengeneza mashine za ndani za kuchakata kakao, siagi ya shea, muhogo,kahawa, na mazao mbalimbali kuwa bidhaa zenye kustawisha Afrika na ulimwengu.
Hapa nazungumzia lugha ya asili ya mwaafrika yenye kubeba asili na urithi wetu ambao ni lugha ya Kiswahili itakayoibua waafrika kuwa wabunifu wa kuboresha maisha ya waafrika.
Mwana wa Afrika kumbuka bara halijengwi na wale wanaochapisha zaidi, bali na wale wanaounda zaidi,wanobuni vitu na kugundua. K**a tuonavyo mataifa mengine k**a china,korea, ujerumani, n.k.
Hebu turudi Kwenye lugha zetu za asili, tuache ubinafsi na kasumba za kikoloni ambazo hazitatusaidia k**a waafrika, tujikite katika uwekezaji wa kubuni na tafiti zenye tija hakika Afrika itajitukuza.
“Mungu ibariki Afrika, Kiswahili lugha yetu”.❣️

21/01/2026
FIKRA ZA LUGHA YA KISWAHILI Ndoto ni upeo wa azimia ya matendo, na fikira ni hadiriki ya kutenda jambo, kwa maana ya taf...
20/01/2026

FIKRA ZA LUGHA YA KISWAHILI
Ndoto ni upeo wa azimia ya matendo, na fikira ni hadiriki ya kutenda jambo, kwa maana ya tafakari ya kujikomboa katika jamii iliyo na sifa ya ukosefu wa hazina. Hapa ndipo ninapokumbuka na kurejelea lugha na mawazo yaliyojitokeza katika kazi za fasihi za Kiafrika, hususani katika fikra za Ngũgĩ wa Thiong'o ambaye alitaka waandishi wajikomboe kutokana na mategemezi makubwa ya lugha za kigeni (hasa Kiingereza, Kifaransa, Kireno na Kihispania) na watumie lugha za Kiafrika. Yeye mwenyewe alikuwa akifanya hivyo kwa kuendelea kuandika kazi zake za kubuni kwa kutumia Gikuyu (lugha yake ya kwanza).
Kwa kufanya hivi Thiong’o amehitimisha malengo matatu:
Kwanza kuzipa hadhi lugha za Kiafrika
Pili kuzuia athari zaidi zinazotokana na lugha za kigeni hasa Kiingereza
Tatu kuonyesha kwamba lugha za Kiafrika (k**a lugha nyingine kuu duniani) zina mchango mkubwa katika kuwasilisha na kufasiri mazingira ya watumizi wa lugha hizi.
Fikra hizi zimeendelea kuzua mjadala mkubwa na hasa wakati huu wa mwingiliano wa jamii barani Afrika na Ulimwenguni.
Kiujumla, lugha mbili tofauti huwasilisha uhalisia tofauti kwa sababu ya tofauti za uzoefu. Tatizo lililopo ni kuwa katika nchi nyingi za Afrika lugha zilizopewa nguvu na uwezo wa kuwakilisha mitazamo na tafsiri za ulimwengu, ni lugha za kigeni ambazo Waafrika wengi wamezipokea k**a lugha za pili au za tatu katika mifumo mbalimbali ya elimu. Cha ajabu ni kwamba ni asilimia ndogo sana ambayo inaweza kudai kwamba inazimudu lugha hizi.
Ili mtu aweze ‘kujikomboa’ kutokana na mtazamo huu wa ulimwengu, ni lazima kwanza ajikomboe kutokana na lugha iliyomfikisha hapo alipo.

Mtafiti ninayemtaja hapa juu aliamini kwamba watu wakishajikomboa au wakishakombolewa kimawazo wataweza kujiendeleza katika nyanja zingine zile zikiwemo kiuchumi, kisiasa, na kijamii. Hivyo Waafrika hatuna budi kuendeleza lugha ya Kiswahili ambayo inatokana na lugha za kibantu na yenye kubeba utamaduni wa Mwaafrika ili tujikomboe. Maana taifa lolote lile ili lifanikiwe linahitaji kutumia lugha yake ya asili mfano nchi zinazotumia lugha zao ni China, Uingereza, Korea,Vietnam, Urusi n.k lakini kinyume chake ni kuendelea kuwa kwenye mnyororo wa chuma.

❣️Mungu ibariki Afrika, Kiswahili lugha yetu❣️

FIKRA ZA KISWAHILI.    🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️ Asubuhi na mapema wengi hujifunika shuka k**a kwamba usiku umebakia kwenye n...
19/01/2026

FIKRA ZA KISWAHILI. 🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️🗣️ Asubuhi na mapema wengi hujifunika shuka k**a kwamba usiku umebakia kwenye njozi zao. Na wachache huamka kwa ajili ya kutofautisha mifuatano ya usiku na mchana. Usiku kuwa ni sehemu ya mapumziko na mchana ni sehemu ya kutafutia maisha”.
Asubuhi namapema niliamka kuenda makataba iliyosheheni mkusanyiko wa kila aina ya maarifa, Niliingia humo na kuanza kulisha akili yangu ambapo nilishaba historia na lugha ya Kiswahili
Nilishangaa kujua kumbe maendeleo haya ya lugha ya Kiswahili tunayoona leo ni matokeo ya juhudi za enzi zilizofanya na viongozi hao wa kijadi na waasisi wa mataifa, Dini,Biashara na mapokeo ya wananchi. Kumbe walianza kufanya biashara, kilimo, ufugaji, utabibu, ualimu, ujenzi na shughuli kadha wa kadha kwa muda mrefu na kwa ujuzi mkubwa sana wakitumia Lugha ya Kiswahili.
Maarifa niliyopata katika maandishi yalinijuza mengi kuyajua ili kupiga mbiu ya mgambo kubomoa fikra potofu ndani ya jamii kuhusu lugha hii.
Mpenzi wa Lugha ya Kiswahili, lugha hii Afrika na duniani kote itaishi ndani ya watu, itabadilika na wakati, na itaendelea kujenga utambulisho, umoja na maendeleo ya Afrika.
Hali hii ndio itakayofanya lugha hii kuaathiri maisha ya Waafrika kila siku katika hali chanya. Vilevile Lugha hii itakuwa daraja la maarifa na elimu ili kuendeleza Afrika na dunia.
Fumba na kufumbua, Nyoyo za wananchi wa Afrika zitakuwa wazi, huru, moja na kuwa baraka kwa mama Afrika. Na mwana wa Afrika atajenga fahari yake ndani ya msingi imara, atajiamini na kujitambua k**a Waafrika wenye lugha yao ya asili.
Hivyo, ni natoa rai yangu Mwana wa Afrika! Mpenzi wa lugha ya Kiswahili! Na wote wenye nia njema na lugha hii, Matumaini yetu ya kuendeleza lugha ya Kiswahili nimeyaweka mabegani mwenu.Ushindi wa lugha ya Kiswahili ninauweka mikononi mwenu. Ufundishaji na kujifunza lugha ya Kiswahili ninauweka midomoni na akilini mwenu na ushindi wa lugha hii upo vichwani mwenu. Jambo hili tunalitarajia kutoka kizazi hiki hadi vizazi vijavyo
“Mungu ibariki Afrika, Kiswahili ni lugha yetu”

17/01/2026

FIKRA ZA KISWAHILI
Ni sauti yenye mvuto ya ndege kutoka mwituni ambayo ilisikika masikio mwangu. Ilivuta fikra zangu kutaka kumjua yule ndege. Lakini punde nilikumbuka shujaa wa lugha ya Kiswahili kutoka nchini Tanzania aliyepata kutoa mwelekeo wenye mafundisho kwa wana waafrika kufuata maadili, maono na maamuzi yenye kubeba hatima ya Afrika.
Shaaban Robert aliandika kazi nyingi sana za fasihi na Alikuwa shujaa na miongoni mwa waandishi waliojenga misingi ya kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili. Katika fasihi yake inaonyesha mwelekeo wa maadili, haki, na utu. Nikiwa katika hali hii ya kumkumbuka, nilikumbuka shairi lake aliloimba: T**i la mama ni 💖 tamu. Hebu kaa katika hali ya kutafakari shairi: Hii ni Shairi la SHAABAN ROBERT:
T**i la mama litamu, hata likiwa la mbwa,
Kiswahili naazimu, sifayo iliyofumbwa,
Kwa wasiokufahamu, niimbe ilivyo kubwa,
Toka k**a mlizamu, funika palipozibwa,
T**i la mama litamu, jingine haliishi hamu’.

Hili ni shairi linalozungumzia jinsi lugha ya Kiswahili ilivyo tamu k**a t**i la mama kwa mtoto wake.
Wana wa Afrika, uwe kiongozi au mwananchi, mwanaharakati au mwanasiasa, Baba au mama, kijana au mzee na wapenzi wote wa Kiswahili ni imani ya mama Afrika kuwa kila mmoja anaamini kuwa lugha yetu ya Kiswahili ni tamu k**a t**i la mama lilivyo kwa mtoto. Hivyo, ni wajibu wa kila mmoja kutoka pande zote za dunia kuendelea
kuienzi lugha hii kwa kuendeleza matumizi yake sahihi na kuonesha umuhimu wake kwa wasioifahamu hata waone hamu ya kuitumia k**a alivyoandika Shaaban Robert.
❣️Mungu ibariki Afrika, Kiswahili lugha yetu❤️

15/01/2026

Boys taking Yoruba History class at The Nigeria Colony Welfare Department Boys Club.

Date: 12/11/1946

Organized welfare homes and formal work structures were first set up in Lagos and Calabar in 1943. That same year, Nigeria’s first Juvenile Court was opened. Remand homes were also created to keep convicted boys who were waiting for trial under the Children and Young Persons Ordinance of 1943.
Approved institutions were later established in Isheri in the Lagos Colony and in Enugu. These welfare centers were designed to care for the boys and help give them a sense of pride and belonging in society.
The Boys’ Hostel on Bola Street, Lagos Island, was opened in October 1947 to provide temporary shelter for waifs and strays. A Girls’ Hostel was also set up in a similar way, and by 1947 the number of girls in the hostel had grown to 629.

Source: The Colonial Office List of 1949 (Physical/ Digital Document available with ASIIR Magazine)

Text Source: © ASIRI Magazine 2025

Image Credit: McKay, Vernon (Collector)/ Herskovits Library of African Studies

Address

Ilala
Dar Es Salaam
55814

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Fikra za Kiswahili posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share