12/05/2026
🚨 *MABADILIKO MAPYA YA MITAALA YA ELIMU SHULE ZA MSINGI, SEKONDARI NA VYUO* 2025
MABORESHO YA MITAALA AMBAYO YANAENDA KUBADILISHA MFUMO WETU WA ELIMU:
1. Mtihani wa darasa la Saba utafutwa ifikapo 2027.
2. Mwanafunzi akianza darasa la kwanza lazima amalize Kidato cha nne. Hii itaitwa Elimu ya Msingi.
3. Kutakuwa na Mtihani wa Upimaji wa Kitaifa wa darasa la sita (STANDARD SIX NATIONAL ASSESSMENT) ifikapo 2026.
4. Mwanafunzi atatakiwa asome fani fulani kabla hajamaliza Kidato cha nne ili aweze kujiajiri au kuajiriwa baada ya kumaliza. Hii itaanzia Secondary ambapo kutakuwa na mikondo miwili; Jumla na Amali.
5. Lugha ya kufundishia na kujifunzia itakuwa kiswahili, Kiingereza kitakuwa k**a somo kwa Shule za Kiswahili Medium na lugha ya kufundishia English, kiswahili kitakuwa K**a somo kwa Shule za English Medium.
6. Elimu ya Msingi itakuwa miaka 6. Mwanafunzi ataanza darasa la kwanza akiwa na miaka 6 tofauti na ya sasa miaka 7.
8. Elimu ya Awali mwanafunzi ataanza akiwa na miaka 5. Mwanzoni elimu ya awali haikuwa rasmi na shule za Serikali haikuwepo. Sasa itakuwepo kwa utaratibu huo.
9. Masomo ya Elimu ya Msingi yatakuwa ni KKK(Kusoma, Kuhesabu, Kuandika), Jiografia, kiswahili, Sanaa na Michezo, Hisabati, Sayansi, historia ya TANZANIA na Maadili, Dini na kiingereza na Stadi za Kazi itachomekwa.
10. Kiingereza kitafundishwa kuanzia darasa la kwanza kwa shule za Kiswahili na kiswahili kitafundishwa kuanzia darasa la kwanza kwanza kwa shule za kiingereza.
11. Shule zenye uwezo zitafundisha angalau somo moja la lugha za kigeni k**a Kichina au Kifaransa.
12. Sekondari kutakuwa na mikondo 2, mkondo wa jumla na Amali (Ufundi). Mwanafunzi atachagua kutokana na uwezo, matakwa na malengo yake ya baadaye.
13. Mkondo wa amali (ufundi) utakuwa na fani zifuatazo:-
> Kilimo na Ufugaji.
> Umakenika.
> Biashara na Ujasiriamali.
> Sanaa na Ubunifu.
> Elimu ya Michezo.
> Ufugaji wa Nyuki.
> Uchimbaji wa Madini.
> Urembo.
14. Mwanafunzi wa Mkondo wa Amali atatakiwa kuchukua Masomo manne (4) ya jumla na moja la fani.
15. Masomo ya jumla ya wanafunzi wa Amali ni:-
> Hisabati.
> Elimu ya Biashara.
> Kiingereza.
> Historia ya Tanzania na Maadili.