15/09/2021
Bishop Patrick Mmeta kwa niaba ya Kanisa la Pentecoste Tanzania natoa salamu zangu za pole kwako na kwa familia yako. Roho ya mama yako(bibi)😭 iwe na amani kwa Baba yetu wa Mbinguni.
Nimesikitishwa sana na habari za kupoteza kwako. Ninaomba kwamba Mungu akupe nguvu. Salamu zangu za dhati kabisa.
Pole sana kwa msiba huu mzito,Mungu akawe mfariji wako wa kweli kwenye kipindi hiki kigumu,nakutakia safari njema Mungu akutunze ufike salama umpumzishe bibi kwenye nyumba yake ya milele..
21/06/2021
Highlights of Sunday Service
UNAWEZAJE KULINDA MOYO WAKO??
Moyo ndiyo chanzo cha uhai wako,moyo wako ukiwa vizuri Mungu anaweza kusema nawewe.
Mithali 4:23
[23]Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo;
Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
Ni jukumu la kila mmoja kutunza moyo ili kuwa na uzima.
JINSI YA KULINDA MOYO
1.Kuweka neno la Mungu kwa wingi ndani yako
-Kwenye neno la Mungu ndiko kuna full package ya kila kitu.
-Kila mkristo ni lazima aweke ratiba ya kusoma neno,likijaa kwa wingi ni rahisi kumshinda shetani.
-Soma neno,kula neno,tafakari neno la Mungu kila wakati,ili tumjue na kumfahamu Mungu ni katika kulisoma neno.
-Neno la Mungu huuisha,hujenga unaposoma hutabaki k**a ulivyo.
-ulinzi wa moyo wako unategemea kiwango chako cha kusoma neno la Mungu.
2.Epuka vikundi vibaya
-jiepushe na mambo/vitu ambavyo vitachafua moyo wako
1 Wakorintho 15:33
[33]Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.
-Sisi tuliomwamini Kristo au tuliokolewa tuna mipaka katika mambo mengi.
Zaburi 1:1
3.Usifikiri mambo ya mwili
Warumi 8:8
[8]Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
-K**a watoto wa Mungu ni lazima tudhamirie kumpendeza Mungu.
-K**a unaufata mwili maana yake ndani yako hakuna Mungu,muombe Mungu akusaidie uwe na muda nayeye.
-Duniani si mahali pa milele kuntafuta Mungu ndiyo maisha ya milele,gharama ya muda itoe ili Mungu atumike nawewe.
Isaya 43:18
4.Rizika na ulichonacho
-Tunatakiwa kurizika kwa namna ya Ki Mungu.
-unaporizika unapata muda wa kumshukuru Mungu.
1 Timotheo 6:6
[6]Walakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa.
-uone ubora wako unapofanikiwa pamoja na kumcha Bwana.
Mithali 15:16
6.Omba mara kwa mara
-Maombi ni ufunguo(master key)
-omba omba omba wakati wote
-Tulinde moyo ili tuishi kwenye kusudi na tutumikie kusudi la Mungu.
-Mtafute Mungu kila wakati ili ulinde moyo wako.
7.Usitawaliwe na mawazo mabaya
-Kataa jambo baya linalokuja kwenye ufahamu wako linalokuja nje ya mapenzi Ya Mungu.
KATIKA JAMBO LOLOTE KUMBUKA ULINZI WA MOYO WAKO NI JUKUMU LA WEWE MWENYEWE,CHANZO CHA UZIMA WAKO INATOKANA NA UWEZO WAKO WA ULIZI WA MOYO WAKO,MUOMBE MUNGU AKUSAIDIE JINSI YA KUUTUNZA MOYO WAKO...
By.Mwl Pendo
Kwa mafundisho ya neno la Mungu karibu kanisani Kipunguni kwa Diwani Dar es salaam MUNGU AWABARIKI SANA 🙏
Mawasiliano tupigiie +255 713 802 120
11/01/2021
HONGERENI WATOTO WA KLPT-Moria Centre,MMEFANYA VIZURI SANA KWENYE SIKUKUU YA WATOTO MUNGU AZIDI KUWAINUA MKAWE WATOTO WENYE MAADILI MEMA MKAWE BARAKA POPOTE MTAKAPOKUWA ,PONGEZI KWENU WAALIMU KWA MAFUNZO BORA KWA WATOTO WETU, WAZAZI PIA TUNAWASHUKURU KWA USHIRIKIANO WENU MUNGU AWABARIKI SANA......
Karibuni wote kanisani kwetu Kipunguni kwa Diwani Dar es Salaam Tz,Ibada zetu ni Jumatatu Jumanne na Ijumaa saa kumi nanusu jioni, Jumapili saa mbili asubuhi nakuendelea piga no +255 713 802 120
MBARIKIWEEEE!!!!
06/01/2021
KUMTUKUZA MUNGU NAYE ATAKUTUKUZA
Na.Askofu Patrick Mmeta
Utangulizi....
Kumtukuza Mungu ni kumwinua/kumpa Mungu utukufu,kumtukuza Mungu ni pamoja na kufanya mambo anayotaka Mungu tufanye(maisha matakatifu,kuwa na hofu na Mungu).
Maisha ya wokovu ni ya mtu mmoja mmoja(kwenda mbinguni ni jambo la mtu binafsi na kila mtu anatakiwa awajibikie kuhakikisha analinda uthamani wa wokovu).Wokovu ni vita.
zaburi 27:10
[10]Baba yangu na mama yangu wameniacha,
Bali BWANA atanikaribisha kwake.
walio na Yesu(waliompokea na kumkiri Yesu) wamepita kutoka mautini wameingia uzimani.
Tulio na Yesu hatupo chini ya mamlaka ya mauti(haimaanishi mauti ya kufa)maisha yetu ni ya uzima hakuna kufeli kwasababu maisha yetu yanasimamiwa na Mungu.
Yohana 5:24
[24]Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani.
FAIDA ZA KUMTUKUZA MUNGU
1. Mithali 4:6-9
[6]Usimwache, naye atakuhifadhi;
Umpende, naye atakulinda.
[7]Bora hekima, basi jipatie hekima;
Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu.
[8]Umtukuze, naye atakukuza;
Atakupatia heshima, ukimkumbatia.
[9]Atakupa neema kuwa kilemba kichwani;
Na kukukirimia taji ya uzuri.
Katika mawazo yako hakikisha umuachi Yesu,ukimtendea mema nayeye anakufanyia mema.
Ili Mungu akuhifadhi inategemea ni kiwangi gani unampenda.
Kutukuzwa na Mungu ni kuinuliwa(jina lako linakuzwa).
2.Atakupatia miaka mingi yenye uzima duniani.
3.Mungu hawezi kukuaibisha ukimtukuza(wanaotaka kukuaibisha wataaibika).
*Kumtukuza Mungu ni pamoja na kutopita njia moja na waovu(wabaya).
mithali 4:14-16
*Kukaa na Mungu ni afya ya mwili na Roho.
Mithali 4:20-22
MAMBO YA KUJIHADHARI NAYO
1.Mithali 4:23
[23]Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo;
Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
Damu ya Yesu na maombi ndiyo yatakayokusaidia kufuta makosa yako,moyoni mwako kusiwe na mawazo mabaya.
2.Kujilinda na moyo wa ukaidi /ulimi(mambo mabaya).
Mithali 4:24
[24]Kinywa cha ukaidi ukitenge nawe,
Na midomo ya upotovu uiweke mbali nawe.
3.Jilinde macho yako yatazame mbele(kujiepusha na uovu usiingie kwenye ufahamu wako).
Mithali 4:25,27
Katika maisha ya wokovu tunahitaji kuwa makini sana ili Mungu atuinue kutoka sehemu moja hadi nyingine,kwenye huduma,kazi,masomo,ndoa na familia zetu tunatakiwa maisha yetu yamtukuze siku kwa siku tumuishi yeye kila wakati....
Mungu akubariki sana....
Karibu kujifunza neno la Mungu lisilogoshiwa kanisani kwetu Kipunguni kwa Diwani jijini Dar es salaam Tanzania,Jumatatu,Jumanne,na Ijumaa saa Kumi na nusu (10.30) jioni...
Kwa maombi,ushauri na maelekezo zaidi piga
+255 713 802 120,+255 712 050 723
03/01/2021
Zaburi 20:8
[8]Wao wameinama na kuanguka,
Bali sisi tumeinuka na kusimama.
NINATANGAZA KATIKA JINA LA YESU BWANA AKUINUE NA USIMAME MWAKA HUU UFANYE MAMBO ULIYOSHINDWA KUFANYA,UFANIKIWE KWENYE BIASHARA,MASOMO,KAZI,NDOA NA CHOCHOTE UFANYACHO....
ADUI ZAKO WOTE WAANGUKE NA KUINAMA KATIKA JINA LA YESU....
Karibuni wote kwenye ibada kwanzia saa 3 asubuhi,kanisa lipo kipunguni kwa diwani jijini dar es salaam,piga no kwa maulizo,maombi au ushauri +255 713 802 120....
UBARIKIWE!!!
01/01/2021
HAPPY NEW YEAR 2021 TO ALL
Zaburi 65:11
[11]Umeuvika mwaka taji ya wema wako;
Mapito yako yadondoza unono.
NATANGAZA K**A KUHANI,UKAWE MWAKA ULIOBEBA MEMA KATIKA NDOA,KAZI,AFYA,MASOMO,BIASHARA NA JUU YA UZAO WA TUMBO LAKO KATIKA JINA LA YESU KRISTO...
NAAMURU KATIKA JINA LA YESU MAPITO YAKO YOTE(chochote utakachofanya) KIFANIKIWE KATIKA JINA LA YESU....
Karibuni nyote kwenye ibada ya kinabii leo kwanzia saa tatu(3) asubuhi upate salamu za kinabii za mwaka mpya...Kanisa lipo Kipunguni kwa diwani jijini Dar es salaam,nipigie kwa maombi,ushauri au maelekezo +255 713 802 120 mimi ni Askofu Patrick Mmeta.
Mbarikiweee!!!!!
24/12/2020
BWANA YESU APEWE SIFA!!
KWA MOYO WA DHATI KABISA NIKUALIKE NDUGU YANGU KATIKA BWANA KWENYE MKESHA WA CHRISMASS,KUMBUKIZI YA KUZALIWA KWAKE YESU KRISTO MWOKOZI WETU KARIBU TUUNGANE KWENYE IBADA,MAOMBI YANGU KWAKO YESU AZALIWE KWA UPYA NDANI YA MOYO WAKO,UTAPOKEA BADILIKO NDANI YA MAISHA YAKO,KANISA LIPO KIPUNGUNI KWA DIWANI JIJINI DAR ES SALAAM.
MKESHA UTAANZA SAA TATU USIKU KARIBUNI NYOTE NA MUNGU AKUBARIKI....
Zaburi 20:1
[1]BWANA akujibu siku ya dhiki,
Jina la Mungu wa Yakobo likuinue.
BWANA AKUJIBU KATIKA MAOMBI YAKO SAA HII MAGUMU YOTE YAWE MEPESI KWA JINA LA YESU
Piga +255 713 802 120 MAOMBI,USHAURI AU MAELEKEZO JINSI YA KUFIKA KANISANI KWETU.....