02/09/2023
Salaam toka Talawanda!
Leo Ijumaa tar 1/9/2023, viongozi wa Talawanda Sekondari, Afisa Elimu Kata, Mkuu wa Shule na Makamu Mkuu wa Shule waliungana na viongozi wenzao katika ukumbi wa Kikwete uliopo kwenye Makao Makuu ya Wilaya katika KIKAO KAZI CHA TATHMINI YA MATOKEO NA KUWEKA MIKAKATI KWA MUDA ULIOBAKI.
Katika kikao hicho waliudhuria viongozi mbalimbali wakiwemo: Mkurugenzi wa Halmashauri ya Chalinze, Mhe Ramadhani Possi, Mkuu wa Idara ya Utumishi Bw *Kilaja Alkanus, Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari Mama Salama Ndyetabura, Maafisa toka Idara ya Elimu Sekondari, Maafisa Elimu Kata wote, Wakuu wa Shule zote, Makamu Wakuu wa Shule, Viongozi wa Idara ya Michezo na Utamaduni pamoja na Sekritarieti ya Michezo Wilaya.
Yaliwasilishwa mengi. Kwa uchache ni tathmini ya KPI, majadiliano ya namna ya kuboresha utendaji kazi na ufaulu, masuala ya kiutumishi, kifedha, elimu maalumu na lishe, maandalizi na ratiba ya mitihani mbalimbali pamoja na namna ya kuboresha michezo mashuleni.
Mkurugenzi aliweka msisitizo kwenye maandalizi ya mitihani ya Taifa pamoja na maandalizi yake. Aliwataka watakaoteuliwa kufuata maelekezo ya semina walizopewa ili wasiharibu kazi. Pia, usimamizi mzuri wa fedha za serikali kwa wenye kupata miradi ili iendane na thamani ya fedha iliyotolewa. Mwisho alitoa pongezi na kuwatakia watumishi kila la heri.
Imetolewa na Idara ya Habari - TSS.