10/11/2021
*PART ONE*
*IFAHAMU SIRI YA MBEGU NA GANDA LA TIKITI MAJI KWA AFYA YAKO MWANADAMU*
Tikiti maji ni moja ya mazao ya kifahari duniani.
Tunda hili ni chanzo kikuu maji na ni muhimu kwa mwili wa binadamu.
Wataalamu wanaelezea tikiti maji k**a tunda ambalo ni muhimu sana kwa afya ya binadamu, kwasababu ina madini ya hali ya juu ya ikiwa ni pamoja ya Vitamini, Midini, Vizuia oksidi na Mafuta.
Kuna aina tano tofauti ya tikiti maji.
Lakini katika mataifa kadhaa ya Afrika, tikiti maji ni tunda maarufu sana.
Tikiti maji lina asilimia 92 ya maji, ikimaanisha kuwa wale wanaotumia tunda hilo hawana hofu ya kukabiliwa na ukosefu wa maji mwilini, anasema mtaalamu wa masuala ya lishe bora Maijidda Badamasi Burji.
Zifuatazo ni faida tisa za tunda la tikiti maji kwa mwili wa binadamu kwa mujibu wa wataalamu:
Inaongeza maji mwilini
Maji ya na umuhimu mkubwa kwa mwili wa binadamu, ndio maana watu wanakunywa maji kwa wingi ili kuboresha afya zao.
Wataalamu wanashauri matumizi ya tunda la tikiti maji ambalo lina asilimia 92 ya maji, utafidia haja ya kunywa maji zaidi.
Tunda hili pia lina madini ya hali ya juu inayosaidia mwili wa binadamu.
Vitamininamadinini mengine
Tikiti maji ni moja ya matunda na mboga ambazo zina kiwango cha chini cha mafuta.
Kiwango cha mafuta katika tunda la tikiti maji kiko chini ikilinganishwa na matunda mengine.
Kikombe kimoja cha maji ya tikiti maji kina madini aina ya Vitamini C, A, Potassium, Magnesium, Vitamini B1, B5 na B6.
0768504232