Saimu Gwao

Saimu Gwao Hii ni Official page ya Mwanahabari mkongwe wa Kiislam nchini Tanzania, Saimu Gwao

*MUFT AFURAHISWA NA NDOA, YA FAMILIAR YA SHEKH KIDAGO NA SHEKH SAMIR, NI JAMBO KUBWA LA KUILINDA  DINI*Na Saimu Gwao Jij...
24/04/2026

*MUFT AFURAHISWA NA NDOA, YA FAMILIAR YA SHEKH KIDAGO NA SHEKH SAMIR, NI JAMBO KUBWA LA KUILINDA DINI*

Na Saimu Gwao
Jijini Tanga
April 24, Saa 11 jioni

Alhamdullilah hadhara ya kihistoria Jijini Tanga imemalizika salama na Muft wa Tanzania alishiriki na kufurahiswa na ndoa hiyo ya wanachuoni hao na kusema huu ni mfano wa kuigwa.

Muft alisema, Jambo la ndoa ni dini,sio ada wengi wanatofautisha ndio maana wanachuoni wanasema ndoa ni katika sababu kubwa ya kulinda dini na Dunia, hii ndio misingi ya dini inavyotaka nimefurahiswa wote wawili walinialika, kwa maana Shekh Yusuf Kidago na Shekh Samir ambapo Leo ndio wameunga rasmi udugu baada ya kuozesha watoto wao.

*MUFT WA TANZANIA AHUDHURIA NDOA YA KIHISTORIA TANGA , SHEKH SAMIR ASEMA ANA FURAHA KUBWA SANA LEO*Na Saimu Gwao Shamsul...
24/04/2026

*MUFT WA TANZANIA AHUDHURIA NDOA YA KIHISTORIA TANGA , SHEKH SAMIR ASEMA ANA FURAHA KUBWA SANA LEO*

Na Saimu Gwao
Shamsul Maarif Tanga
April 24 Saa 8 mchana

Muft wa Tanzania katika harusi ya kihistoria ya kijana wa Shekh Yusuf Kidago ambae amemuoa mtoto wa Shekh Samir Leo mara baada ya swala ya ijumaa, ndoa iliyofungwa na mwenyewe baba wa bibi harusi Shekh Samir Sadik

Ambapo amesema ana furaha kubwa sana Leo kwa kumuozesha bint yake, kwa mtoto wa Shekh Yusuf Kidago ambae nae ni mwanae, Kijana wake na pia amefurahi sana mtoto wake kuolewa na mtoto wa Shekh Yusuf Kidago, tuko live Saimu Gwao tv.
Muda huu ...

Mashekh na wanawazuoni mbalimbali wamehudhuria kiasi kwamba Shekh Samir amewashukuru sana na kusema hawezi kuwataja wote kwa kuwa ni wengi sana, ila hakukosa kulitaja jeshi la mtu mmoja Shekh mziwanda na Shekh Kaporo ambae toka Jana Yuko hapa.

*KUMEKUCHA TAASISI YA ITRAVEL HAJJ AND UMRA KUANZA RASMI SEMINA ZA HIJJA JUMAMOSI HII, NYOTE MNAKARIBISWA*Na Saimu Gwao ...
16/04/2026

*KUMEKUCHA TAASISI YA ITRAVEL HAJJ AND UMRA KUANZA RASMI SEMINA ZA HIJJA JUMAMOSI HII, NYOTE MNAKARIBISWA*

Na Saimu Gwao
April 17/ 2026.
Mumbai nchini India

Kumekucha Sasa, kuelekea katika ibada ya Hijja 2026, Taasisi ya ITravel Hajj & Umrah, inatarajiwa kuanza rasmi semina za mahujaji kwa muda wa wiki nne kuanzia 18/04/2026, chini ya usimamizi wa Mwanachuoni Shekh Twaha Suleiman Bane..

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na mratibu Mkuu wa maswala ya Hijja wa Taasisi ya ITravel Hajj & Umrah, Sheikh Juma Kijepa, ni kwamba masomo yatakua kila siku jumamosi na jumapili kwa kila wiki.
Na masomo yatakayo somehswa ni:-
Maana ya ibada ya Hijja, na umuhimu wake, nguzo zake na wajibu wake, mbali na hayo pia kutakuwa na adabu za safari, maana ya Umrah.

Mbali na Shekh Twaha Bane, pia atakuwepo Sheikh.Muaharram Mwaita Mkurugenzi wa Africa Tv Swahili, na Shekh Yusuf Machalenga, Shekh Juma Kijepa, pamoja na Mkurugenzi Mkuu Ahmed Sharif.

Semina zitafanyika katika Msikiti wa Mwinyimkuu Magomeni Mapipa Jijini Dar es Salaam, na Mahujaji wa taasisi zote wanaruhusiwa kuhudhuria semina hiyo kwaajili ya kuijua mapema ibada ya hijja ili wasipate tabu wakiwa Makka.

Ni kawaida kwa taasisi ya ITravel na taasisi zingine kuanza mapema semina za hijja, tayaari taasisi ya Jamaraty , Tawheed, Al Safaa , Al istaqama na zingine zimekwisha anza semina za hijja.

Semina hiyo huwa inaanza saacTatu asubuhi mapema kabisa na kwa wale waliokuwa Mikoani , mtapata matukio yote kupitia Saimu Gwao tv.
Darul Arcam tv
Arcas tv.

Tutakuwa live bila chenga.

*KUMEKUCHA KUELEKEA HIJJA 2026, VIONGOZI WAKUU WA TAASISI YA ITRAVEL HAJJ AND UMRAH WAKUTANA KUJADILI MAANDALIZI YA SAFA...
28/03/2026

*KUMEKUCHA KUELEKEA HIJJA 2026, VIONGOZI WAKUU WA TAASISI YA ITRAVEL HAJJ AND UMRAH WAKUTANA KUJADILI MAANDALIZI YA SAFARI YA HIJJA-2026*

Na Saimu Gwao
Masjid Mtoro Dar
March 28/2026

Kumekucha mambo ya Hijja yameiva kwa mwaka huu wa 2026, viongozi wakuu wa Taasisi ya ITravel Hajj and Umrah wamekutana Leo katika kikao cha kawaida kujadili na kutafakuri matayarisho ya hHjja 2026.

Kikao hicho kilichoongozwa na Mkurugenzi Mkuu Mr.Ahmed Sharif, kilijadili juu ya kuanza rasmi kwa mafunzo au semina ya Hijja yanayotarajiwa kuanza mwezi ujao 18/4/2026.
Semini zitakasomeshwa na Mwanachuoni:-
1. Shekh Twaha Suleiman Bane.
2. Shekh Juma Kijepa.
3. Shekh Yusufu Machalenga.
Na semina hii huwa inafanyika katika Msikiti wa Mwinyimkuu Magomeni Mapipa Jijini Dar es Salaam

Kwa upande mwingine semina za Zanzibar zinatarajiwa kuanza wiki ijayo Tarehe 6/4/2026.
kwa mujibu wa Ustadh Sabri na Takdir na wengineo, miongoni wa wasimamizi wakuu wa Taasisi ya ITravel Zanzibar.

Viongozi waliohudhuria katika kikao cha Leo ni:-
1. Shekh Juma Kijepa.
2. Shekh Yusufu Machalenga.
3. Shekh Abdulramid Rwezaula kutoka Mutukula Kagera.
4. Pamoja na mkurugenzi Mkuu Ahmed Sharif.

HAYA KUMEKUCHA, KUMEKUCHA, MZIGO WA MAANA KABISA KWA MAANA KANZU ORIGINAL ZA WATOTO COTTONI ZENYEWE HIZI, ZINAPATIKANA M...
28/02/2026

HAYA KUMEKUCHA, KUMEKUCHA, MZIGO WA MAANA KABISA KWA MAANA KANZU ORIGINAL ZA WATOTO COTTONI ZENYEWE HIZI, ZINAPATIKANA MASJID MTORO DUKANI KWA SAIMU GWAO TU. KWA UFUPI WAHI MAPEMA NASIKITIKA KUSEMA ZIPO CHACHE SANAA HIVYO MWENYE KUWAHI AU KUBAHATIKA BEI YAKE HIZO NI ELFU 45 MWISHO SAIZI HAMSINI NI ZA WATOTO TU ZAIDI WASILIANA NA SAIMU GWAO 0713471090 KWA WHATSAP POPOTE UTATUMIWA

25/02/2026

Sheikh Othman Maalim

Anatualika katika Mashindano Makubwa zaidi ya Qur’aan Tukufu ya Mabara Yote Ulimwenguni, yanayoandaliwa na Al-Hikma Foundation chini ya usimamizi wa

Yatafanyika tarehe 01/03/2026 Uwanja wa Mkapa , Kuanzia Saa 12 Asubuhi - Saa 7 Mchana
*Ndani ya Ramadhaan* Dar es Salaam Tanzania
*NAOMBA USAMBAZE* 👏

25/02/2026
25/02/2026

*WATU WA TANGA WANAANZA SAFARI KWA BAJAJI*

*WEWE WA JIJI LA GHARAMA WASUBIRI NINI!!?*

*TAASISI YA ITRAVEL HAJI AND UMRAH YAFUNGA SEMINA YA HIJJA ZANZIBAR LEO, PIA IMEKWISHAJAZA MAHUJAJI WA 2026, SASA TUNAWA...
15/02/2026

*TAASISI YA ITRAVEL HAJI AND UMRAH YAFUNGA SEMINA YA HIJJA ZANZIBAR LEO, PIA IMEKWISHAJAZA MAHUJAJI WA 2026, SASA TUNAWAPOKEA WA 2027 TU*

Na Saimu Gwao
Kijiji cha Tiku lushoto
Feb 15 Saa 12 Jioni

Taasisi ya ITravel Hajj And Umrah leo feb 15/2026 wamefunga rasmi semina ya ibada ya Hijja visiwani Zanzibar, baada ya kuendeswa semina hiyo kwa muda wa zaidi ya miezi mitatu.

Shekh Juma Kijepa Mratibu mkuu wa maswala ya Hijja kupitia Taasisi ya ITravel leo aliwashukuru Mahujaji hao watarajiwa na kuwapa somo muhimu la adabu za safari na Ustadh Musadik nae aligusia hijja kwa ufupi, huku mahujaji wakiwa na shauku kubwa wakiyahisabu masiku ya hijja k**a mwezi wa Ramadhani.

Taasisi ya ITravel ambayo utaratibu wake wa kufanya semina za hijja mapema visiwani Zanzibar na kufanya ziara za kuhimiza ibada ya hijja imepelekea kujaza mapema watu sana mwaka huu tokea January, tumekwishafunga rasmi dirisha la usajili wa hijja kwa 2026, hivi sasa tumeanza kusajili Mahujaji wa 2027.

Kumekuwepo na uhitaji mkubwa kwa mwaka huu watu kutaka kusafiri na Taasisi ya ITravel Hajj and Umrah lakini kutokana na sintofahamu tulipewa idadi ya watu wa mwaka jana 65 tu, wakati sisi tulihitajia watu 100.

Semina iliyofungwa leo Zanzibar, Inshaa'Allahu itafunguliwa tena mara baada ya sitta shawal
Na kwa upande wa Tanzania bara pia semina zitaanza rasmi mara baada ya kumalizika Mwezi wa Ramadhani.

*KUMEKUCHA YALE MAHAFALI YA CHUO CHA AL MISBAH, ILALA SASA KUFANYIKA KESHO JUMAPILI, UKUMBI WA DYCC*Na Saimu Gwao Mavumo...
14/02/2026

*KUMEKUCHA YALE MAHAFALI YA CHUO CHA AL MISBAH, ILALA SASA KUFANYIKA KESHO JUMAPILI, UKUMBI WA DYCC*

Na Saimu Gwao
Mavumo lushoto
Feb 14 Saa 2 Asb

Alhamdullilah mambo yameiva sasa yale mahafali ya chuo cha Al Misbah Islamia kilichopo Ilala Jijini Dar, sasa rasmi mahafali yake yanafanyika kesho siku ya jumapili feb 15/2026 katika ukumbi wa Dyccc Wilaya ya Temeke Jijiini Dar

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa chuo hicho Shekh Asbat Said Suleiman ni kwamba maandalizi yote yamekamilika, ambapo shughuli hiyo inatarajiwa kuanza mapema siku ya kesho saa mbili asubuhi.

Viongozi wa Serikali pamoja na mashekh na Viongozi wengine wa Taasisi mbalimbali za kiislam wanatarajiwa kuhudhuria katika mahafali hayo.

Kwa upande mwingine Shekh Asbat amewapongeza sana wazazi, wnafunzi pamoja na walimu kwa kuonyesha ushirikiano mkubwa sana pamoja ns maendeleo mazuri ys wanafunzi kila mwaka.

Mahafali hayo yanashirikisha wanafunzi wa elimu ya thanawi na diproma yanayotolewa chuoni hapo.

Zaid kwa mawasiliano na Shekh Asbat Said Suleiman
0778337085
Hadhara hiyo inatarajiwa kuwa live
Saimu Gwao tv

*KUMEKUCHA MUFT WA TANZANIA KUZINDUA RASMI, BUSART LA MTORO JUMANNE FEB 17,SHEKH ABBAS ASEMA MAANDALIZI YOTE YAMEKAMILIK...
12/02/2026

*KUMEKUCHA MUFT WA TANZANIA KUZINDUA RASMI, BUSART LA MTORO JUMANNE FEB 17,SHEKH ABBAS ASEMA MAANDALIZI YOTE YAMEKAMILIKA*

Na Saimu Gwao
Magamba lushoto
Feb 12 Saa 8 Mchana

Kumekucha kile kipindi pendwa cha Busart la Mtoro kinachofanyika kila mwezi wa Ramadhani kinatarajiwa kuzinduliwa rasmi siku ya Jumanne feb 17/2026 na Muft wa Tanzania Dk Shekh Abubakar Zuber.

Kwa mujibu wa Imam mkuu wa Msikiti wa Mtoro Shekh Abbas Ramadhan, maandalizi yote yamekamilika kwa wanawazuoni wa East Afrika ambapo zaidi ya mada 25 zinatarajiwa kuwasiliswa.

Shekh Hamid Masoud Jongo, Shekh Twaha Suleiman Bane, Yusuf Kidago Shekh Samir Sadik, Shekh Izudini Alwi, Sharif Abdulqadir,Shekh Shams Elmy na wengine wengine wanatarajia kuwasilisha mada.

Kipindi cha Busart la Mtoro ni kipindi pendwa sana karibia watu Dunia nzima kutokana na umahiri wa uendeshaji wake kupitia Imam Mkuu wa Msikiti wa Mtoro Shekh Abbas Ramadhan akishirikiana na wenzake, Shekh Abdallah Almundhir pamoja na Shekh Othman Khamis ambapo huwa kinaruswa kupitia ZBC TWO na Dua tv pekee.

Address

Mahiwa Na Livingstone

00255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Saimu Gwao posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

  • Want your school to be the top-listed School/college?

Share