07/02/2024
Mshikamano VTC katika ushirikiano na chuo kikuu cha Maendeleo ya Jamii TICD ,Tumeungana na kufanya mdahalo wa kitaaluma juu ya mada mbalimbali katika kuibua changamoto zinazoikabili jamii na kuzitafutia ufumbuzi.
Mada zilizojadiliwa zilijikita katika changamoto za ukatili wa kijinsia na kujitambua kwa vijana hasa wanafunzi.
Mdahalo huu ulifanyika katika chuo cha MSHIKAMANO VTC 05/02/2024 na kuwahusisha wanafunzi, waalimu pamoja na maofisa kutoka kitengo cha utafiti na machapisho yanayohusu wanawake (NWRDC) Kilicho chini ya TICD .