Toto la Mbura

Toto la Mbura

Share

Living a live in Christ.In Him am ok

23/11/2024

Mama aliniambia, mwanangu Kila siku ni siku ya makuzi. Siku ya kurindima aushi na kupiga hatua pachapacha kwa makuzi. Ila pia kila tarehe ishirini na tatatu mwezi wa Novemba pasi ya mwaka ni siku ya kuvuka mwaka.Dah! Mungu daima asaidia. Kesho kwema kwa vile Mungu yupo. Siku heri ya kizaliwa Toto la Mbura 😊🍹

07/11/2024

LISILOBADILIKA MABADILIKO

Daima naishi kusikia kuwa kuinamako ndiko kuinukako. Je kuinukako bado ndiko kuinamako? Hilo swali tu la balagha. Tuishipo daima lisilobadilika ni mabadiliko. Mengine yote ni mabadiliko yanayobadilika badilika kila kutokeako mabadiliko. Naam, hata miamba hubadilika ikawa mchanga, nyumba ikawa ganjo, miti ikawa mbao, mtu akawa marehemu, mchana ukuwa usiku, giza likawa mwanga.
Hivi nasemani? Naufananisha ulimwengu na jangwa ambapo hapawezi pakachipua lolote. Ila, hata jangwa likinyunyiziwa chemichemi ukuza mazao na kubadili eneo likawa chanikiwiti. Ndipo nikasema lisilobadilika, basi ni mabadiliko tu.
Namaanishani? Tuishipo si ajabu mja kurithishwa taabu na masaibu. Akasalia hana hanani, akiulizwa haungami. Hiyo ndiyo hali halisilia. Kuruba na msukosuko wa maisha ukamkandamiza kiasi cha kujuta kuishi. Akatamani laiti isingekuwa ilivyo. Ila lisilobadilika ni mabadiliko tu.
Kwa hilo, ukirithishwa taabu na masaibu, pambana kubadilisha angalau uwe na mwisho mwema, kwani hata hadithi za Riwaya licha wa muhusika mkuu kuteseka, mara nyingi huishia kwa mwisho mwema. Tupambane
Zaidi ya yote, tusichukiane. Tusisemane vibaya. Tusikadamizane. Tusiumizane. Tusidharauliane. Tusitakiane mabaya. Tusiharibiane mapambano. Daima tusaidiane. Tusisahau kuwa msaada ni kikoa, ukisaidiwa nawe saidia mwingine.
Kesho kwema, kwa vile Jalia yupo.






Mwandisha, mwigizaji,mwanahabari,muhubiri

02/11/2024

NINA ALINIAMBIA

Nina alimbi, 'Kijanangu kwenye aushi hii, usije ukakata tamaa. Huenda ikawa leo ni pagumu na pia mbele paonekana pagumu ila tumaini lisikosekane. Kwa vile likisokena basi kiza kitatanda. Kiza kinene.' Hivi alimaanisha nini? Machache ya kuyangamua yapo.
La kwanza. Daima si Kila wakati Leo huwa pema. Ila pa mbele si Kila wakati hutamanika. Daima maisha ni sawa na swali lisilo na jibu. Pia ni sawa maishani kuwa upo katika njia usiyoijua Leo na hata kesho hujui itakuwa vipi. Hivi nasema ni? Kuwa maisha ni sawa ni sawa na kusafiri katika njia isiyoijua.
La pili, licha ya yote, tumaini lisikose. Safari lazima isonge. Yakizibika, zidi kuzibua. Yakifungana, zidi kufungua. Tumaini daima iwe kichocheo cha kuendesha gurundumu la maisha.
Daima nenda bila kukuma. Kaza Tumaini maishani. Fanya ufanyacho kwa tumaini kamili

08/10/2024

MAAJABU YA AJABU

Wanasema tunaishi kwenye ulimwengu wa malimwengu. Dunia rangi rangile eti. Dunia ya maajabu. Mengine ata yamebaki mafumbo yaliyotugeuza wajinga kwa kutoweza kuyafumbua. Lakini maajabu ya ajabu nimeyashuhudia mara kadha. Tena yana ajabu ya ajabu kwa vile yamejaa ya ajabu ambayo si ajabu kuyasataajabia.
Hivi nasema nini? Ni ajabu kwamba walio wa uwezo wa kubadirisha mambo na ata kuibandilisha nchi, wanakosa hari, kujiamini, kujituma, kupiga hatua na wanaishia bure bilashi.
Lakini la ajabu zaidi, wasio na uwezo wanayafanya haya yote na kuishia kufanikiwa. Haya si maajabu?
Wamaanisha nini nawe Toto la Mbura? Hivi namaanisha kwamba sababu ya ukiritimba, uchochole, ugumu wote huu wa maisha, ni kwa vile tumelalisha bongo. Hivi umejiuliza una uwezo upi wa kuboresha hali? Na ulipojua umetenda lipi? Ama wangoja lipi litendeke dio ufanye jambo?
Watasema kwamba hawana uzoefu, hawana hela, hawana rasilimali. Aaaah! Hivo vijisababu tu. Bongo lako ni kila kitu. Anguka nayo. Twende nalo

kwema
la mbura
ziwa kuu jangwani
kave baharini
kisiwani
mwana wa Ali

22/05/2024

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Bahati Kirema Samson, Sam Sammy Okombo, Mike Douglas, Mercie Mercie

15/05/2024

THEY DON'T KNOW

Some times I ask myself why don't people help others to succeed. Why don't they give a support when needed? Even if you plead and explain, they don't. Why?
A simple answer is because they don't know. Yes, they don't know what exactly you want. You vision, dream and aim is so big that they can ever understand. Its is only you who knows want you want.
So just do want you know will make you succeed and never wait for anyone to help you. Since they don't know.

12/05/2024

They say, a mother is like a Gold. I say, my mother is more than a gold. The most precious person ever. The conqueror, the best of bests. Whe they all left, ahe never left. Happy mothers day mum❤️🥰.

16/04/2024

Jamani wenzangu, naomba tuache kutumia mihandarati. Hivi kijana jirani yangu amepiga mtindi, sasa hivi anawahadithia wazazi wake alivyokuwa kwa shida kubwa akiwa yatima asiye na mama wala baba😅😅. Mie sijui pombe ikiisha kichwani atasema nini😂😂

14/04/2024

Ndovu ameanguka😂😂

FT Arsenal 0 - Aston villa 2

24/01/2024

Wega ngugene. Swali la siku. Ni nini hasa huwa inafanyika wapenzi wanaanza kukosana? Na kuona k**a kulikuwa na makosa kukubali kuingia kwa mahusiano? Yaani, nini humaliza s**e ya mahusiano? Nena nami

22/01/2024

Its on a Monday. Hivi weekend ilikuwa aje? Nini kilikufurahisha au kukukasirisha? Nena nami.
Wega FM 88.6. 10am to 2pm

16/01/2024

Kunani kule Roma? Aliyewahi kunoa Totenham, Manchester united, Chelsea na hata Real madrid, ametimuliwa kule As Roma. Ati kusudi ni matokeo mabovu.
The special is now among unemployed people

courtesy.

Want your school to be the top-listed School/college in Meru?

Click here to claim your Sponsored Listing.

Location

Telephone

Website

Address

Meru

Opening Hours

06:00 - 19:00