18/06/2025
Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe Lakagua Magari ya Shule Kwa Lengo la Kuimarisha Usalama wa Wanafunzi
Njombe, 18 June 2025
Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe leo limeendesha zoezi maalumu la ukaguzi wa magari yanayotumika kusafirisha wanafunzi wa shule mbalimbali mkoani hapa, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuhakikisha usalama wa wanafunzi barabarani.
Zoezi hilo limefanyika katika viunga vya shule ya msingi bakita mkoani Njombe likisimamiwa na KAIMU RTO NJOMBE SP-DAUDI DAUDI MAPUNDA na INSP H.HAULE ,S/SGT RAFAEL NA H.5549 CPL TEODORY WAKAGUZI WA MAGARI NJOMBE.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa zoezi hilo, KAIMU RTO amesema kuwa ukaguzi huo umelenga kutathmini hali ya usalama wa magari, vibali vya usafirishaji, na sifa za madereva wanaoendesha magari hayo.
“Tunakagua hali ya matairi, breki, taa, kioo cha mbele, vyeti vya usajili, leseni za madereva, pamoja na vifaa vya dharura k**a vizima moto, k**a hatua ya kuhakikisha kuwa wanafunzi wanasafirishwa katika mazingira salama,” alisema kaimu RTO.
Magari yalibainika kuwa na kasoro mbalimbali ikiwemo breki zilizochoka, matairi yaliyotoboka, na ukosefu wa vifaa vya usalama k**a “first aid kit” na vizima moto yameelekezwa kufanyika kwa marekebisho mapema na kukaguliwa tena baada ya matengenezo na marekebisho.
Magari yenye kasoro hizo yamezuiwa kwa muda hadi marekebisho yatakapofanyika, huku wamiliki wa magari hayo wakipewa maelekezo ya kurekebisha kasoro hizo mara moja.
Jeshi la Polisi limetoa wito kwa wamiliki na waendeshaji wa shule kuhakikisha kuwa magari yao yanatunzwa vyema, kufanyiwa matengenezo ya mara kwa mara, na kuendeshwa na madereva wenye sifa na uelewa wa sheria za usalama barabarani.
“Hili ni jukumu la pamoja kati ya Serikali, shule na wazazi. Tunatoa wito kwa shule zote kuhakikisha madereva wao wanapitia mafunzo ya usalama barabarani na magari yote yanakaguliwa mara kwa mara,” aliongeza SP-DAUDI DAUDI MAPUNDA.
Jeshi la Polisi limeahidi kuendeleza zoezi hili kila baada ya miezi mitatu, huku likiahidi kushirikiana na mamlaka za elimu na usafirishaji kuhakikisha kila gari linalotumika kubeba wanafunzi linazingatia viwango vya kiusalama.
Aidha, limewataka wazazi kuwa makini na namna watoto wao wana